Muhoozi awatishia shemeji zake, kisha 'awasamehe'
Mzozo wa kifamilia watokea katika familia ya Rais wa Uganda Yoweri Museveni na kuenea hadharani kiwango cha Mkuu wa Mejeshi ya nchi hilo kutishia kumkamata shimeji wake.
Jenerali Muhoozi Kainerugaba ambaye ni mkuu wa majesty Uganda, na Mtoto wa Rais Museveni kupitia mtandao wa X Mapema siku ya Ijumaa alizungumza kwa ukali akimkashifu shemeji yake drek Rwabwogo ambaye ni mume wa Askofu Patience Museveni Rwabogo.
amesema kwamba atazungumza na dada zake wawili Patience na Natasha kutatua mzozo uliopo.
Rwabogo aidha ni mshauri mwandamizi wa Rais Museveni na mwenyekiti wa Kamati inayoshughulikia mauzo ya nje na maendelo ya kiviwanda nchini Uganda.(PACEID)
Kwa mujibu wa vyanzo nchini Uganda Mvutano kati ya Muhoozi na Rwabwogo umekuwa ukidhirika wazi kwa mda mrefu.
Lakini umeingia katika awamu nyingine baada ya Muhoozi kumtuhumu Rwabwogo kwa ‘ufisadi’ na kutishia kumkamata huku akitaja kamati ya PACEID kama ilio kinyume cha sheria.
Katika machapisho yake kwenya mtandao wa X, Muhoozi pia aliandika na kumkana Shemeji huyo na alilazimishwa tu na wazazi wake kumkubali. Katika ujumbe huo alimtaja shimeji yake mwingine Edwin Karugire kuwa kipenzi chake na kwamba maoni ya Watoto wa kiume yanapswa kuheshimiwa na wazazi hasa kuhusu ndoa za mabinti wao.
Rwabwogo amewahi kukosoa kile alichokiita kutokuwapo kwa uwajibikaji na vikwazo dhidi ya uhuru wa kiraia nchini Uganda.
Wafuasi wao pia wamekuwa wakizozana hadharani-ila kwa sasa, majibizano kati ya hao wawili yanazidi kuakisi mvutano mpana zaidi kuhusu ushawishi wa kisiasa na suala la urithi wa uongozi ndani ya mfumo tawala wa Uganda.