Khamenei: Nilikubali makubaliano baada ya kupewa uhakikisho kuhusu maslahi ya Iran
Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ametoa ujumbe mpya kuhusu makubaliano yaliyofikiwa kati ya Iran na Marekani, akisema alikubali mpango huo licha ya kuwa na msimamo tofauti hapo awali.
“Nilikuwa na mtazamo tofauti kimsingi. Hata hivyo, kwa kuwa Rais wa Iran, kama mkuu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, aliniahidi kwa niaba yake na wanachama wengine wa baraza hilo kwamba haki za wananchi wa Iran na Muungano wa Upinzani zitalindwa, na akakubali wazi kuwajibika kwa hilo, nilitoa idhini yangu,” alisema Khamenei.
Wakati huo huo, Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) imethibitisha kuondolewa kwa mzingiro wa majini uliokuwa umewekwa dhidi ya meli zote zinazoingia au kutoka katika bandari za Iran.
Katika taarifa yake, CENTCOM ilisema operesheni zote za kijeshi za kutekeleza mzingiro huo zimesitishwa na kwamba vikosi vya Marekani havitazuia wala kuingilia harakati za meli zinazoelekea au kutoka katika bandari za Iran kwenye Ghuba.
Hata hivyo, meli zitakazopita katika Mlango wa Hormuz zitalazimika kufuata mfumo wa uratibu wa Iran, kwa mujibu wa Baraza la Usalama la Taifa la Iran.
Vyombo vya habari vya serikali ya Iran viliripoti kuwa ushuru na ada zilizokuwa zikitozwa meli zimesitishwa, huku Iran ikikubali kugharamia ada hizo ndani ya siku 60 kama sehemu ya waraka wa makubaliano uliotiwa saini kati yake na Marekani.
Licha ya hatua hiyo, meli bado zitalazimika kuwasilisha maombi kwa mamlaka mpya ya mamlaka ya ghuba ya uajemi , chombo kilichoanzishwa na Iran wakati wa vita ili kuimarisha udhibiti wa njia hiyo muhimu ya majini.
Kwa upande wake, Rais wa Marekani Donald Trump amesema anatarajia usitishaji wa mapigano kutekelezwa katika maeneo yote ya mzozo, ikiwemo Lebanon na mapigano kati ya Israel na Hezbollah.
Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wake wa Truth Social, Trump alisema anatumaini mataifa ya Mashariki ya Kati “yatatekeleza ahadi zao ili kuwezesha mazungumzo yetu kuendelea.”
Pia unaweza kusoma: