Watu 10 wajeruhiwa baada ya Urusi kuishambulia Kyiv
Watu 10 wamejeruhiwa baada ya Urusi kuishambulia mji Kyiv, nchini Ukraine, kwa makombora ya balistiki mapema hii leo.
Shambulio hilo limefanyika wakati Kyiv inasubiria kupokea vifaa vipya vya ulinzi wa anga, huku kukiwa na uhaba ambao umeacha mji huo katika hatari zaidi ya mashambulizi ya Urusi.
Kulingana na shirika la habari la Reuters, raia wa mi huo aliwaambia kuwa alisikia milipuko kadhaa mikubwa katika jiji hilo mwendo wa alfajiri kabla ya tahadhari ya mashambulizi ya anga kutolewa na Ukraine.
Jeshi la anga la Ukraine limesema Urusi ilirusha makombora sita ya balistiki, makombora sita ya masafa marefu na ndege 121 zisizo na rubani.
Jeshi hilo limesema liliweza kudungua angalau makombora mawili ya masafa marefu na ndege zisizo na rubani 111 zilizokuwa zikilenga maeneo mbalimbali nchini humo.
Soma pia: