Moja kwa moja, Israel yasema imefanya mashambulizi ya anga yaliyolenga maeneo ya magharibi na katikati ya Iran

Hakukuwa na maelezo zaidi yaliyotolewa kuhusu idadi ya walioumia au waliouawa, wala maeneo halisi yaliyolengwa katika mashambulizi hayo.

Skip Video and continue reading
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Lizzy Masinga

  1. Maandamano yafanyika Tehran

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Tunapata baadhi ya picha sasa za maandamano yanayoiunga mkono serikali yanayoendelea Tehran, kufuatia mashambulizi ya Israel kwenye viunga vya kusini mwa Beirut.

    Wengi wa waandamanaji kwenye picha wamebeba bendera za Iran na Hezbollah, kundi la kisiasa na kijeshi linaloungwa mkono na Iran nchini Lebanon.

    .

    Chanzo cha picha, AFP

    .

    Chanzo cha picha, AFP

  2. Bei ya mafuta yapanda baada ya Iran kurusha makombora dhidi ya Israel

    .

    Chanzo cha picha, Anadolu via Getty Images

    Bei ya mafuta imepanda Jumatatu asubuhi barani Asia baada ya Iran kurusha makombora dhidi ya Israel kwa mara ya kwanza tangu kufikiwa kwa makubaliano ya usitishaji vita kati ya nchi hizo na Marekani mwezi Aprili.

    Bei ya kimataifa ya mafuta ghafi ilipanda kwa 2.6% hadi $95.50 (£71.60) kwa pipa, wakati mafuta yasiyosafishwa ya Marekani yalipanda kwa 2.5% hadi $92.75.

    Bei za nishati zimekuwa na mabadiliko makubwa tangu makubaliano ya kusitisha mapigano Aprili yalipokubaliwa.

    Bei zimepanda kwa karibu $95 katika wiki iliyopita huku wafanyabiashara wakipima athari za muda mrefu za vita dhidi ya mtiririko wa nishati duniani.

  3. Ripoti za vifo na majeruhi kutokana na tetemeko Ufilipino bado zinathibitishwa

    Uharibifu

    Chanzo cha picha, Philippine Red Cross

    Kumekuwa na ripoti za vifo kutokana na tetemeko Ufilipino, ingawa bado hazijathibitishwa rasmi.

    Mamlaka zinaendelea kuthibitisha takribanivifo vitano vilivyoripotiwa, kulingana na shirika la habari Reuters.

    Afisa mmoja wa polisi ameiambia AFP kwamba mtu mmoja amethibitishwa kufariki na wengine wanne wamejeruhiwa.

    Diego Mariano, afisa wa taarifa kutoka wakala wa kitaifa wa majanga wa Ufilipino, amesema kuwa ripoti za vifo na majeruhi zinafuatiliwa kwa karibu.

    Pia kuna taarifa za uharibifu mkubwa katika miundombinu mbalimbali.

    Ameonya wananchi kuepuka kurudi ndani ya nyumba zao au majengo mengine, hasa yale yanayoonesha dalili za uharibifu.

    Unaweza kusoma;

  4. Trump asema Netanyahu hatakuwa na jinsi, isipokuwa kukubali yatakayoafikiwa

    Trump

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Trump amesema kwamba Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu “hatakuwa na chaguo lingine” isipokuwa kukubali makubaliano yoyote ambayo Marekani itafikia na Iran.

    Akizungumza na Financial Times kupitia simu, Trump alisema: “Yeye hatakuwa na jinsi. Mimi ndiye ninayeamua. Mimi ndiye ninayeamua kila kitu. Yeye (Netanyahu) si anayeamua.”

    Trump pia aliiambia Axios hapo awali kwamba atamuomba Netanyahu asiendelee kulipiza kisasi dhidi ya Iran baada ya mashambulizi ya hivi karibuni, ili kuhakikisha pande hizo tatu zinaweza kufikia makubaliano.

    Kwa mujibu wa Financial Times, Trump alisema mashambulizi ya hivi karibuni hayajabadilisha chochote kuhusu mchakato wa makubaliano.

    “Tutaona jinsi itakavyomalizika,” alisema Trump.

    Unaweza kusoma;

  5. Tetemeko kubwa la ardhi limekumba eneo la kusini mwa Ufilipino

    Tetemeko

    Chanzo cha picha, Philippine Institute of Volcanology and Seismology

    Tetemeko kubwa la ardhi limetokea kusini mwa Ufilipino saa majira ya saa moja na dk 37 kwa saa za eneo hilo.

    Kwa sasa ukubwa halisi na kina cha tetemeko hilo bado havijathibitishwa kikamilifu.

    Kulingana na Taasisi ya Ufilipino ya Volkeno na Matetemeko ya Ardhi (Phivolcs), tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa 7.0 na kina cha kilomita 10 (maili 6.2).

    Hata hivyo, Shirika la Utafiti wa Jiolojia la Marekani (USGS) limeripoti ukubwa wa 7.8 na kina cha kilomita 35, huku Kituo cha Utafiti wa Jiolojia cha Ujerumani kikiripoti ukubwa wa 7.8 na kina cha kilomita 50.

    Nchi kadhaa za eneo hilo, zikiwemo Ufilipino, Indonesia na Japani, zimetangaza tahadhari za tsunami.

    Unaweza kusoma;

  6. Israel imesema imefanya mashambulizi ya anga yaliyolenga maeneo ya magharibi na katikati ya Iran

    Moshi mzito

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Israel imesema imefanya mashambulizi dhidi ya maeneo ya magharibi na katikati ya Iran.

    “Dakika chache zilizopita, Jeshi la Anga la Israel lilishambulia maeneo ya kijeshi yanayomilikiwa na utawala wa kigaidi wa Iran katika maeneo ya magharibi na katikati ya Iran,” Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) limesema kupitia Telegram.

    Hakukuwa na maelezo zaidi yaliyotolewa kuhusu idadi ya walioumia au waliouawa, wala maeneo halisi yaliyolengwa katika mashambulizi.

    Katika hatua nyingine, Televisheni ya taifa ya Iran sasa inaripoti milipuko katika miji mitatu baada ya Israel kusema jeshi lake la anga limefanya mashambulizi dhidi ya maeneo ya kijeshi katikati na magharibi mwa Iran.

    “Milipuko kadhaa imeonekana kusikika Tehran, Tabriz na Isfahan,” televisheni ya taifa imeandika kupitia Telegram.

    Milipuko pia imeripotiwa kusikika karibu na mji wa kati wa Karaj.

    Taarifa hizi zinakuja wakati hali ya tahadhari ikiendelea kuongezeka kutokana na mfululizo wa mashambulizi kati ya Israel na Iran, huku maelezo zaidi yakitarajiwa kutolewa.

    Unaweza kusoma;

  7. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu.