Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Je, ni wachezaji gani matajiri zaidi wa soka duniani?
Ni miaka 10 imepita tangu Cristiano Ronaldo awe mwanasoka wa kwanza kuwa bilionea.
Alipoondoka Real Madrid kwenda Juventus, bahati yake ilifikia kilele. Kisha akatajwa kuwa bilionea.
Ronaldo kwa sasa anaingiza zaidi ya dola milioni 300 kwa mwaka. Anafuatiwa na Lionel Messi.
Karim Benzema ni wa tatu na anapata $104 milioni kwa mwaka. Kylian Mbappé ndiye anayefuata akiwa wa nne kwa dola milioni 95. Haya ni mapato ya mwaka mmoja tu, na yanajumuisha mshahara pamoja na ridhaa mbalimbali.
Lakini ni nani mchezaji wa kandanda tajiri zaidi duniani?
1. Christian Ronaldo
Amepata na kufikia kiwango cha juu kabisa cha mafanikio ya binadamu katika soka. Hata akiwa na umri wa miaka 41, kiu yake ya mafanikio ni ya ajabu.
Hata leo klabu yake ikishindwa analia. Kupoteza na kukata tamaa sio tabia ya Ronaldo.
Kwake hakuna kilichosalia kwa mpira wa miguu isipokuwa kushinda Kombe la Dunia.
Anaweza kufanya hivyo katika nchi yake ya Ureno kwenye Kombe la Dunia la mwaka huu, ambalo linaandaliwa kwa pamoja na Marekani, Mexico na Canada.
Alikua katika hali ngumu sana; baba yake, ambaye hakuwa na chakula, wakati mwingine alimwomba pizza, kwa sababu ya mzigo wa kifedha wa familia.
Cristiano Ronaldo ni mmoja wa mabilionea duniani leo.
Pia alinunua 25% ya timu ya daraja la pili ya Uhispania UD Almería.
Alipata utajiri wa kujenga hoteli za kifahari nchini Ureno, na pia anamiliki mojawapo ya makumbusho yaliyotembelewa zaidi huko Lisbon.
Anamiliki ndege binafsi na idadi ya magari ya gharama kubwa. Tangu kuhamia Al Nassr, anapata karibu pauni milioni 200 kwa mwaka. Pia anapata pesa nyingi kutokana na mikataba ya kuidhinisha na Nike na chapa ya CR7.
Kulingana na jarida la Forbes, utajiri wake wote unakadiriwa kuwa takriban dola bilioni 1.4.
2- David Beckham
Mchezaji wa zamani wa Uingereza na Manchester United, David Beckham, amekuwa mwanariadha wa kwanza wa Uingereza kuingia kwenye orodha ya mabilionea.
Kwa mujibu wa jarida la Sunday Times Rich, utajiri wa Beckham na mkewe Victoria Beckham kwa pamoja umefikia pauni bilioni 1.185.
David Beckham pia ni mmiliki wa Inter Miami CF, ambayo ina thamani ya karibu £1.45 bilioni.
Pia amefanya kazi na chapa kuu kama Adidas na Hugo Boss kama balozi wa chapa.
Mkewe Victoria Beckham pia huchangia sehemu kubwa ya mapato ya familia, hasa kupitia uanamitindo na usanifu wa mavazi.
3. Lionel Messi
Inasemekana hakuna mchezaji kama yeye katika historia ya soka. Ameshinda kila kitu, ikiwa ni pamoja na Kombe la Dunia.
Akiwa amechezea FC Barcelona, Paris Saint-Germain, na sasa Inter Miami CF, Lionel Messi amevunja rekodi nyingi katika ligi mbalimbali. Amecheza mechi 64, akifunga au kusaidia mabao 100.
Hakuna mchezaji mwingine katika Ligi Kuu ya Soka ambaye amefikia kiwango hiki akiwa na mechi chache.
Mwaka huu, inasemekana alipata dola milioni 28.3, zaidi ya timu 28 za ligi kwa pamoja.
Ameisaidia Inter Miami CF kushinda mataji katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake.
Anamiliki ndege binafsi na magari mengi ya kifahari ya gharama kubwa.
Mapato yake hayaishii kwenye mshahara pekee, lakini pia anapokea mikataba mikubwa ya uidhinishaji kutoka kwa Adidas na Apple TV. Pia inasemekana kuwa Al Hilal SFC imempa mshahara mkubwa.
Hivi majuzi alinunua nyumba huko Barcelona yenye thamani ya $13 milioni.
Utajiri wa Lionel Messi ni zaidi ya dola bilioni 1, na pia amesaini mkataba wa kusalia na Inter Miami CF.
4- Neymar
Neymar amekuwa mtu wa kuvutia sana tangu ajiunge na FC Barcelona. Alikua milionea akiwa na umri mdogo sana. Neymar, ambaye aliufurahisha ulimwengu kwa maisha yake ya soka akiichezea Barcelona pamoja na Lionel Messi na Luis Suárez, tangu wakati huo amejiunga na Paris Saint-Germain kwa mkataba ulioweka rekodi ya dunia.
Baada ya kuondoka PSG, alisaini mkataba wa miaka miwili na Al Hilal SFC, ambao ulisemekana kuwa na thamani ya hadi pauni milioni 400 kwa mwaka.
Licha ya majeraha ya muda mrefu, bado alipata mamilioni ya dola katika mshahara na mikataba ya kuidhinisha.
Neymar pia anajihusisha na biashara, haswa katika nyumba na ujenzi. Kampuni yake ya NR inajihusisha na shughuli mbalimbali za biashara.
Yuko kwenye mkataba wa kuidhinisha wenye thamani ya takriban dola milioni 30 na Puma, na pia anafanya kazi na makampuni makubwa kama Red Bull.
Kulingana na Forbes, jumla ya utajiri wake ni zaidi ya dola milioni 350.
5- Kylian Mbappe
Kylian Mbappé alizaliwa katika familia ya michezo. Baba yake anatoka Cameroon na mama yake anatoka Algeria, na pia alikuwa mpenda michezo.
Kylian Mbappé alianza kulipwa mshahara mkubwa alipokuwa na umri wa miaka 17, alipohama kutoka AS Monaco kwenda Paris Saint-Germain kwa dili kubwa lililoripotiwa kuwa takriban pauni milioni 180.
Anasemekana kuwa na mali na uwekezaji wenye thamani ya mamilioni ya dola, ingawa ripoti za pesa taslimu dola milioni 250 hazijathibitishwa kivyake.
Kylian Mbappé sasa anachezea Real Madrid CF baada ya kuondoka PSG.
Benzema
Huenda Karim Benzema asisifiwe kwa staili yake ya soka.
Lakini alipokuwa Real Madrid hakusifiwa sana kwa sababu kulikuwa na Ronaldo na Gareth Bale. Lakini alifanya vyema dhidi ya wote wawili mwishoni na alionyesha aina ya mchezo wake.
Benzema pia alikuwa akipokea mshahara mkubwa Real Madrid. Kwa vile aliondoka ghafla kwenda Al-Ittihad, alikuwa akipata mshahara mkubwa.
Al Etihad, alikuwa akipata zaidi ya dola milioni 100 kwa mwaka. Anakuza kampuni za manukato kama vile Asafi na Riif.
Hii inaleta jumla ya mali yake kufikia $220.
Zlatan Ibrahimovic ana thamani ya $190 milioni, Wayne Rooney ana $170 milioni, na Erling Haaland ana thamani ya $100 milioni.
Kwa sasa Mohamed Salah ni mmoja wa wachezaji wa Kiafrika wanaolipwa pesa nyingi zaidi na anakadiriwa kuwa na utajiri wa dola milioni 90.