Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Mshukiwa wa shambulio la Washington ashitakiwa kwa jaribio la mauaji dhidi ya Trump

Wachunguzi wanasema mwanamume huyo wa California mwenye umri wa miaka 31 alitaka kuwaua maafisa wengi iwezekanavyo wa ngazi ya juu.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Afisa wa Marekani: Trump hajaridhika na pendekezo la Iran

    Afisa mmoja wa Marekani alisema siku ya Jumatatu kuwa Rais Donald Trump hakuridhishwa na pendekezo la Iran la kumaliza vita kwa sababu halikuzungumzia mpango wa nyuklia wa Iran.

    Shirika la habari la Reuters lilimnukuu afisa huyo wa Marekani akisema, akimzungumzia Trump: "Hapendi pendekezo hili."

    Mapema Jumatatu, Trump alijadili pendekezo hilo na washauri wake wakuu wa usalama wa kitaifa.

    Mzozo wa Marekani na Iran umesalia palepale huku usambazaji wa nishati kutoka eneo hilo ukipungua.

    Vyanzo vya habari vya Iran vilisema mapema Jumatatu kwamba pendekezo hilo litaahirisha majadiliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran hadi vita vitakapoisha na mizozo inayohusiana na urambazaji kutoka Ghuba kutatuliwa.

    Tangu mwanzoni Washington imesisitiza kuwa masuala ya nyuklia lazima yashughulikiwe.

    Vyanzo vya habari kutoka Pakistan, vikifanya kazi kama mpatanishi, viliripoti kuwa juhudi za kukomesha uhasama kati ya Marekani na Iran hazijakoma.

    Hata hivyo, matumaini ya kufufua mazungumzo ua amani yamefifia tangu Trump atangaze wikendi iliyopita kwamba anaahirisha ziara ya mjumbe wake maalum Steve Wittkopf na mkwe wake Jared Kushner mjini Islamabad, mji mkuu wa Pakistan.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Idadi ya watu walionyongwa Korea Kaskazini iliongezeka sana wakati wa janga - ripoti

    Utekelezaji wa hukumu ya kifo uliongezeka sana nchini Korea Kaskazini wakati wa janga la Covid-19, kulingana na shirika lisilo la kiserikali la Seoul.

    Kuanzia Januari 2020 hadi mwishoni mwa 2024, takribani watu 153 walinyongwa au kuhukumiwa kifo - ongezeko kubwa kutoka kwa watu 44 katika miaka mitano kabla ya janga hilo, kulingana na ripoti ya Transitional Justice Working Group (TJWG).

    Baadhi ya makosa yalihusiana na dini, ushirikina na maudhui ya kitamaduni ya kigeni - ikiwa ni pamoja na utumiaji wa tamthilia za K na K-pop.

    Idadi ya mauaji ilipungua kati ya 2015 na 2019 kufuatia shinikizo la kimataifa kufuatia uchunguzi wa kihistoria wa Umoja wa Mataifa.

    Lakini mauaji yaliongezeka mnamo 2020, baada ya Pyongyang kufunga mipaka yake, ilisema TJWG.

    Shirika hilo lisilo la kiserikali liligundua kuwa mauaji nchini Korea Kaskazini yalifikia kilele mwanzoni mwa miaka ya utawala wa Kim, huku zaidi ya watu 80 wakinyongwa mwaka 2013.

    Idadi hiyo inaonekana kupungua kufuatia uchunguzi wa Umoja wa Mataifa ambao uligundua kuwa Pyongyang ilikuwa ikitekeleza ukiukaji wa haki za binadamu kimfumo.

    Maelezo zaidi:

  3. Meli ya kifahari ya Urusi yapitia Hormuz licha ya Mlango huo wa Bahari wa kufungwa

    Meli kubwa inayohusishwa na mmoja wa washirika wakuu wa Rais wa Urusi Vladimir Putin imepitia Mlango-Bahari wa Hormuz, licha ya njia hiyo muhimu ya baharini kufungwa.

    Meli ya kifahari ya Nord, yenye urefu wa mita 142, inayohusishwa na bilionea wa Urusi Alexey Mordashov, ilisafiri kutoka Dubai hadi Muscat, Oman mwishoni mwa juma, mojawapo ya meli kadhaa za kibinafsi zilizovuka bahari hiyo katika miezi ya hivi karibuni.

    Iran imeshirikiana na Urusi katika mazungumzo ya ngazi ya juu wiki hii huku mzozo kati yake na Marekani kuhusu kufunguliwa tena kwa mlango huo wa bahari ukiendelea.

    Takriban moja ya tano ya usambazaji wa mafuta ghafi na gesi asilia (LNG) husafirishwa kupitia njia ya majini.

    Mordashov, ambaye ana uhusiano wa karibu na Putin, hajaorodheshwa kama mmiliki rasmi wa meli hiyo ya kifahari. Lakini, rekodi za Nord zinaonyesha kuwa ilisajiliwa kwa kampuni inayomilikiwa na mkewe mnamo 2022.

    Nord, anayekadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola milioni 500, aliondoka Dubai Ijumaa usiku na kufika Al Mouj, marina katika mji mkuu wa Oman, Jumapili asubuhi, kulingana na data za jukwaa la Marine Traffic.

    Usafiri wa baharini kupitia mkondo wa Ghuba kwa sasa iko katika sehemu ndogo ukilinganisha na viwango vya kabla ya vita.

    Mzozo huo umechangia kupanda kwa kasi kwa bei ya mafuta duniani, huku kiwango cha kimataifa cha mafuta ghafi ya Brent kikipanda hadi dola 109 za Kimarekani kwa pipa siku ya Jumatatu.

    Iran imeendelea kudhibiti usafiri wa meli kupitia njia hiyo muhimu ya majini baada ya Rais Donald Trump kutangaza kuwa vikosi vya Marekani vitaweka kizuizi cha kijeshi dhidi ya bandari za Iran.

    Pia unaweza kusoma:

  4. Mshukiwa wa shambulio la Washington ashtakiwa kwa jaribio la mauaji dhidi ya Trump

    Mtu mmoja mkaazi wa Californiameshtakiwa kwa jaribio la kumuua Rais wa Marekani Donald Trump katika tukio ambalo limeibua maswali kuhusu usalama katika Ikulu ya White House.

    Cole Tomas Allen, 31, pia alishitakiwa kwa makosa mawili ya kupatikana na silaha alipofikishwa mbele ya mahakama mjini Washington DC siku ya Jumatatu.

    Alikuwa amebeba bunduki ya otomatiki, bunduki ya kusukuma maji na visu vitatu alipokuwa akipita eneo la ukaguzi wa usalama kwenye wakati wa dhifa ya Waandishi wa Habari cha White House siku ya Jumamosi, waendesha mashtaka wanasema.

    Afisa wa maalum wa ulinzi alijeruhiwa wakati wa shambulio hilo. Mshitakiwa anakabiliwa na kifungo cha maisha gerezani akipatikana na hatia.

    Akiwa amevalia ovaroli ya bluu yeenye alama ya jina, mshukiwa alionekana mtulivu katika mahakama ya Jumatatu katika mji mkuu wa taifa hilo. Alizungumza kwa upole huku akijibu karibu kila swali kutoka kwa hakimu kwa kutumia maneno "ndio, kwa heshima yako" au "hapana, kwa heshima yako".

    Aliifahamisha mahakama umri wake na kuongeza kuwa alikuwa na shahada ya uzamili.

    Wachunguzi wanasema mwanamume huyo wa California mwenye umri wa miaka 31 alitaka kuwaua maafisa wengi iwezekanavyo wa ngazi ya juu.

    Wakati wa tukio la Jumamosi usiku, Trump, Makamu wa Rais JD Vance, wajumbe wa baraza la mawaziri na maafisa wengine wa Ikulu ya White House waliondolewa kwenye ukumbi wa hoteli ya Washington Hilton baada ya milio ya risasi kusikika.

    Soma zaidi:

  5. Karibukwa matangazo ya moja kwa moja.