DR Congo yaahhidi kuhamisha ubalozi wake wa Israel mjini Jerusalem
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza siku ya Alhamisi kuwa itahamishia ubalozi wake nchini Israel hadi Jerusalem, ikijiunga na kundi dogo la nchi, ikiwemo Marekani, katika kuchukua hatua hiyo yenye uzito wa kidiplomasia ya kuunga mkono mamlaka ya Israel juu ya mji huo mtakatifu wenye utata.
Kufuatia ziara ya Rais Felix-Antoine Tshisekedi, nchi hizo mbili zilisema katika taarifa kuwa zitachukua hatua za "kuhamisha ubalozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutoka Tel Aviv hadi Jerusalem", bila kutaja muda maalum wa kufanyika kwa hatua hiyo.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa, katika mkutano wao, Tshisekedi na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu walizungumzia "nia yao ya pamoja ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia".
Soma pia: