Manchester United inaonesha nia
ya kumsajili mlinzi wa Newcastle United na timu ya taifa ya England, Lewis Hall
(21), ambaye anaripotiwa kutaka kuondoka klabuni hapo.
Mlinzi wa kushoto wa Fulham na timu
ya taifa ya Marekani, Antonee Robinson (28), pia anatazamwa na Manchester
United kama usajili wao kwa msimu ujao.
Barcelona haitalingana na ofa
kubwa za kifedha zinazotolewa kwa kiungo wa Ureno Bernardo Silva (31) na
Atletico Madrid pamoja na Real Madrid, ambazo zote zinataka kumsajili mkataba
wake na Manchester City utakapoisha mwishoni mwa Juni.
Real Madrid inaonekana kuwa mbele
katika mbio za kumsajili Bernardo Silva na tayari ipo kwenye mazungumzo ya
hatua za mwisho kuhusu makubaliano binafsi ya mchezaji huyo.
Beki wa Croatia wa Manchester
City, Josko Gvardiol (24), ameibuka kuwa chaguo kuu la Jose Mourinho kwa ajili
ya kuimarisha safu ya ulinzi ya Real Madrid.
Kocha wa zamani wa Manchester
United, Ruben Amorim (41), anawindwa na AC Milan, ambao wanaamini anaweza
kuleta nguvu mpya katika timu hiyo.
Barcelona inatarajiwa kukataa
fursa ya kumsajili mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford (28) kwa
ada yake ya kuachiliwa ya pauni milioni 26, huku kipengele hicho kikitarajiwa
kuisha muda wake Jumatatu.
Manchester United pia inaweza
kuelekeza nguvu zake kwa kiungo wa Lens, Mamadou Sangare (23), baada ya
kushindwa kumudu gharama za kumsajili kiungo wa England Elliot Anderson (23)
kutoka Nottingham Forest.
Beki wa Borussia Dortmund na
Ujerumani, Nico Schlotterbeck (26), ameweka pembeni mawazo ya kuhamia Real
Madrid ili kuzingatia kwanza FIFA World Cup.
Trabzonspor inataka kukamilisha
usajili wa moja kwa moja wa mlinda lango wa Cameroon wa Manchester United, Andre
Onana (30), msimu huu wa kiangazi.
Manchester United pia inatafuta
kuwaondoa mlinda lango Altay Bayindir (28) wa Uturuki na Radek Vitek (22) wa Czech
Republic, ambaye alikuwa kwa mkopo katika Bristol City msimu uliopita.
Sunderland imejiunga na mbio za
kumsajili mshambuliaji chipukizi wa Bosnia, Kerim Alajbegovic (18), kutoka Red
Bull Salzburg.
Wolverhampton Wanderers inaweza
kuvutiwa kumrejesha mshambuliaji wa West Ham United, Pablo (22), kufanya kazi
tena na kocha mpya Cesar Peixoto, ambaye aliwahi kufanya naye kazi Gil
Vicente FC.
Real Madrid inatafuta kumtoa kwa
mkopo mshambuliaji wa Argentina Franco Mastantuono (18) kwenda Juventus.