Moja kwa moja, Marekani yaishambulia tena Iran, Tehran yajibu

Marekani imedai kuzuia mashambulizi ya Iran baada ya kudungua makombora ya balistiki na ndege zisizo na rubani zilizokuwa zikielekea Mlango wa Hormuz pamoja na nchi jirani za Ghuba ya Uajemi.

Skip Video and continue reading
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Beldeen Waliaula

  1. Timu ya soka ya Iran yapokea viza za kuingia Marekani

    Timu ya Soka ya Iran

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Timu ya Soka ya Iran

    Timu ya taifa ya soka ya Iran imepokea viza za kuingia Marekani kabla ya mashindano ya Kombe la Dunia yatakayoanza wiki Ijayo

    Vibali hivyo vimetolewa siku 10 tu kabla ya mechi yao ya kwanza dhidi ya New Zealand, inayotarajiwa kuchezwa Los Angeles tarehe 15 mwezi Juni.

    Taarifa iliyotolewa na maafisa inasema “Viza zimetolewa kwa Iran kushiriki Kombe la Dunia, ikijumuisha wanamichezo na wasaidizi wao”

    Taarifa hiyo iliongeza kuwa “Marekani haitaruhusu timu ya Iran kutumia mfumo huu kuingiza magaidi nchini Marekani kwa kisingizio cha uongo.”

    Shirikisho la soka la Iran bado halijatoa taarifa rasmi kuhusu kupokea viza hizo.

    Mashindano ya Kombe la Dunia 2026 yanatarajiwa kuanza tarehe 11 mwezi Juni, wenyeji wa mechi hizo wakiwa Marekani, Canada na Mexico.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Putin akataa kukutana ana kwa ana na Zelensky

    Picha ya Vladimir Putin

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Picha ya Vladimir Putin

    Rais wa Urusi, Vladimir Putin amesema haoni haja ya kukutana na rais wa Ukraine VlodymyrZelesnky, baada ya kiongozi huyo wa Ukraine kutaka kufanya mazungumzo ya ana kwa ana, ili kumaliza vita kati ya mataifa hayo mawili.

    Zelensky alikuwa ameandika barua siku ya Alhamisi akitaka kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Putin akisema “ni vibaya kusubiria” vita hivi vilivyoanza na Urusi kuvamia Ukraine mwaka wa 2022 kuangaziwa ten ana Marekani.

    Rais wa Ukraine pia alitaka kuwepo na usitishaji mapigano.

    Putin alijibu barua hiyo akisema ni ya “kifedhuli” na kukataa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na Zelensky na kusisitiza kuwa mazungumzo lazima yafanyike kabla ya usitishaji mapigano.

    “Sioni maana ya mkutano huo” Alijibu Putin alipoulizwa iwapo atakubali mwaliko wa Zelensky

    Baada ya kuskia jibu la Putin, Zelensky alisema “Putin amechagua vita tena, hataki kumaliza vita, na dunia imesikitishwa na jibu lake”

    Pia unaweza kusoma:

  3. Rais wa Colombia, Petro aishutumu Marekani kwa kuingilia uchaguzi wa nchi hiyo

    s

    Chanzo cha picha, CBS

    Rais anayemaliza muda wake nchini Colombia, Gustavo Petro, ameishutumu Marekani kwa kuingilia uchaguzi wa nchi hiyo baada ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kumuunga mkono mgombea wa mrengo wa kulia Abelardo de la Espriella.

    Akizungumza na CBS News, Petro alisema uungwaji mkono huo kutoka kwa Trump ni kitendo cha kuingilia masuala ya ndani ya Colombia, wakati taifa hilo likijiandaa kwa duru ya pili ya uchaguzi wa urais, itakayofanyika wiki mbili zijazo.

    Trump alionyesha wazi kumuunga mkono Abelardo de la Espriella kupitia mitandao ya kijamii na kusema matokeo ya uchaguzi huo ni muhimu kwa mustakabali wa Colombia na uhusiano wake na Marekani.

    Petro amesema tofauti kati ya serikali yake na Washington zinatokana na misimamo ya kisiasa, akidai Marekani imekuwa ikiipinga serikali yake kwa sababu ni ya mrengo wa kushoto.

    Kauli hizo zinakuja huku ushindani mkali ukiendelea kati ya mgombea huyo wa mrengo wa kulia na seneta wa mrengo wa kushoto, Iván Cepeda, kuelekea uchaguzi wa marudio nchini Colombia.

  4. Iran ni nchi yenye kiburi- Trump

    Picha ya Donald Trump

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Picha ya Donald Trump

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema Iran bado haijakubali makubaliano yaliyopendekezwa na Washington kwa sababu ni nchi yenye “nguvu” na “kiburi” na ndiyo maana sio rahisi kwao kukubali matakwa ya Marekani.

    Trump alisema hayo akijibu maswali ya wanhabari.

    Aidha kiongozi huyo aliongezea kuwa Iran imebakisha takriban 22% ya akiba yake ya makombora, na Marekani inaufahamu wa maeneo yaliyoko makombora hayo yaliyosalia pamoja na ndege zisizo na rubani.

    Rais huyo wa Marekani alisema vituo vingi vya kutengeneza makombora, na maeneo ya kurushia silaha nchini Iran vimeharibiwa, ingawa Iran bado ina idadi fulani ya makombora na ndege zisizo na rubani.

    Trump alikiri kuwa kuafikia makubaliano na Iran imekuwa jambo gumu ila bado anamatumaini la hilo kutokea.

    Pia unaweza kusoma:

  5. Marekani yaishambulia tena Iran, Tehran yajibu

    AFP

    Chanzo cha picha, AFP

    Jeshi la Marekani limesema limedungua ndege nne zisizo na rubani za Iran zilizokuwa zikielekea Mlango bahari wa Hormuz, na kudai kuwa yalikuwa tishio la moja kwa moja kwa usafiri wa majini eneo hilo na mataifa mengine ya Ghuba ya Uajemi.

    Kituo kikuu cha kuendesha oparesheni za Marekani za Kijeshi (CENTCOM) imesema kuwa baada ya kudungua ndege hizo, vikosi vya Marekani vilishambulia vituo vya rada za ufuatiliaji vya Iran katika eneo la Goruk na Kisiwa cha Qeshm ili kuzuia mashambulizi zaidi.

    Iran ilijibu hatua ya Marekani kwa kurusha makombora ya balistiki na kulenga kambi za kijeshi za Marekani zilizoko Kuwait na Bahrain.

    CENTCOM imesema kati ya makombora saba ya Iran yaliyolenga nchi hizo mbili za Ghuba, sita yalidunguliwa huku moja haikufikia lengo lake.

    Pia unaweza kusoma:

  6. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja