Timu ya soka ya Iran yapokea viza za kuingia Marekani

Chanzo cha picha, Reuters
Timu ya taifa ya soka ya Iran imepokea viza za kuingia Marekani kabla ya mashindano ya Kombe la Dunia yatakayoanza wiki Ijayo
Vibali hivyo vimetolewa siku 10 tu kabla ya mechi yao ya kwanza dhidi ya New Zealand, inayotarajiwa kuchezwa Los Angeles tarehe 15 mwezi Juni.
Taarifa iliyotolewa na maafisa inasema “Viza zimetolewa kwa Iran kushiriki Kombe la Dunia, ikijumuisha wanamichezo na wasaidizi wao”
Taarifa hiyo iliongeza kuwa “Marekani haitaruhusu timu ya Iran kutumia mfumo huu kuingiza magaidi nchini Marekani kwa kisingizio cha uongo.”
Shirikisho la soka la Iran bado halijatoa taarifa rasmi kuhusu kupokea viza hizo.
Mashindano ya Kombe la Dunia 2026 yanatarajiwa kuanza tarehe 11 mwezi Juni, wenyeji wa mechi hizo wakiwa Marekani, Canada na Mexico.
Pia unaweza kusoma:














