Israel yatangaza wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya Hezbollah
Jeshi la Israel limesema limeanzisha wimbi jipya la mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo walioko wapiganaji wa Hezbollah kusini mwa Lebanon.
Jeshi la Israel awali lilitoa ilani ya kuwahamisha wakazi wa maeneo ya kusini mwa Lebanon.
Mashambulizi hayo mapya yamejiri siku moja tu baada ya wawakilishi wa Israel na Lebanon kukutana mjini Washington na kukubaliana kuongeza muda wa usitishaji mapigano kwa siku 45.
Awali, maafisa wa Lebanon waliishutumu Israel kwa kulenga vituo vya matibabu na wahudumu wa afya
Wizara ya Afya ya Lebanon ilitangaza kuwa Israel ilishambulia kituo cha kutoa msaada na kuwaua watu sita, wakiwemo wahudumu watatu wa afya.
Israel imekanusha kuwalenga wanaotoa misaada na vituo vya afya.
Pia unaweza kusoma: