Moja kwa moja, Trump: Natarajia makubaliano ya kusitisha mapigano yaheshimiwe katika pande zote, ikiwemo Lebanon

Bado hakuna makubaliano kuhusu suala la nyuklia la Iran, ambalo limekuwa na utata kwa muda na kuahirishwa katika makubaliano ya hapo awali.

Muhtasari

Skip Video and continue reading
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid & Asha Juma

  1. Ukatili unaweza kutokea hivi karibuni katika jiji la El Obeid, Sudan

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Muungano wa zaidi ya nchi 20 umeonya kuhusu hatari inayoweza kutokea ya ukatili mkubwa nchini Sudan, ukisema kuwa hadi raia 500,000 wanaweza kuwa katika hatari huku vurugu zikiongezeka karibu na mji wa El Obeid katika eneo la North Kordofan.

    Muungano wa Kuzuia Ukatili na Kuendeleza Haki nchini Sudan ulisema kuwa takriban raia 50 wameuawa katika kipindi cha siku kumi mfululizo za mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika El Obeid na kaskazini mwa Kordofan.

    Pia ulitaja “taarifa za kuaminika za vurugu zinazolenga makundi ya kikabila ikiwemo unyanyasaji wa kingono na wa kijinsia,” na kuonya kuwa zaidi ya watu 100,000 waliokimbia makazi yao ndani ya nchi wanaweza kuwa hatarini ikiwa mapigano yataongezeka.

    "Tunatoa wito kwa Vikosi vya Rapid Support Forces (RSF) kusitisha mara moja mashambulizi yao dhidi ya El Obeid," muungano huo ulisema, huku ukiwataka wahusika wote kupunguza mivutano na kuzingatia sheria za kimataifa za kibinadamu.

    Pia ulitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuongeza shinikizo kwa pande zote zinazopigana ili kuzuia ukatili zaidi.

    Onyo hilo linakuja wakati Umoja wa Mataifa pia umeonyesha wasiwasi kuhusu taarifa za uwezekano wa mashambulizi ya ardhini dhidi ya mji huo, ambao ni mojawapo ya vituo muhimu zaidi vya misaada ya kibinadamu na biashara nchini Sudan.

    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, na Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu, Volker Türk, wote wameelezea wasiwasi wao kuhusu hali inayoendelea kuzorota.

    "Katibu Mkuu ameshtushwa na taarifa za uwezekano wa mashambulizi ya ardhini yanayoweza kutokea muda wowote huko El Obeid," msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stéphane Dujarric, alisema katika taarifa.

    El Obeid ipo kwenye njia muhimu inayounganisha maeneo yanayodhibitiwa na RSF huko Darfur na maeneo yanayodhibitiwa na jeshi mashariki mwa Sudan. Mji huo pia ni kitovu muhimu cha usafirishaji wa misaada ya kibinadamu katika eneo lote la Kordofan. Aidha, inahifadhi idadi kubwa ya watu waliokimbia makazi yao kutokana na mapigano katika maeneo mengine ya Sudan.

    Soma zaidi:

  2. Khamenei: Nilikubali makubaliano baada ya kupewa uhakikisho kuhusu maslahi ya Iran

    n

    Chanzo cha picha, Roberto Schmidt/Getty Images, Iran President Press Office / Handout /Anadolu via Getty Images

    Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ametoa ujumbe mpya kuhusu makubaliano yaliyofikiwa kati ya Iran na Marekani, akisema alikubali mpango huo licha ya kuwa na msimamo tofauti hapo awali.

    “Nilikuwa na mtazamo tofauti kimsingi. Hata hivyo, kwa kuwa Rais wa Iran, kama mkuu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa, aliniahidi kwa niaba yake na wanachama wengine wa baraza hilo kwamba haki za wananchi wa Iran na Muungano wa Upinzani zitalindwa, na akakubali wazi kuwajibika kwa hilo, nilitoa idhini yangu,” alisema Khamenei.

    Wakati huo huo, Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) imethibitisha kuondolewa kwa mzingiro wa majini uliokuwa umewekwa dhidi ya meli zote zinazoingia au kutoka katika bandari za Iran.

    Katika taarifa yake, CENTCOM ilisema operesheni zote za kijeshi za kutekeleza mzingiro huo zimesitishwa na kwamba vikosi vya Marekani havitazuia wala kuingilia harakati za meli zinazoelekea au kutoka katika bandari za Iran kwenye Ghuba.

    Hata hivyo, meli zitakazopita katika Mlango wa Hormuz zitalazimika kufuata mfumo wa uratibu wa Iran, kwa mujibu wa Baraza la Usalama la Taifa la Iran.

    Vyombo vya habari vya serikali ya Iran viliripoti kuwa ushuru na ada zilizokuwa zikitozwa meli zimesitishwa, huku Iran ikikubali kugharamia ada hizo ndani ya siku 60 kama sehemu ya waraka wa makubaliano uliotiwa saini kati yake na Marekani.

    Licha ya hatua hiyo, meli bado zitalazimika kuwasilisha maombi kwa mamlaka mpya ya mamlaka ya ghuba ya uajemi , chombo kilichoanzishwa na Iran wakati wa vita ili kuimarisha udhibiti wa njia hiyo muhimu ya majini.

    Kwa upande wake, Rais wa Marekani Donald Trump amesema anatarajia usitishaji wa mapigano kutekelezwa katika maeneo yote ya mzozo, ikiwemo Lebanon na mapigano kati ya Israel na Hezbollah.

    Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wake wa Truth Social, Trump alisema anatumaini mataifa ya Mashariki ya Kati “yatatekeleza ahadi zao ili kuwezesha mazungumzo yetu kuendelea.”

    Pia unaweza kusoma:

  3. Kombe la Dunia 2026: Canada waidhalilisha Qatar iliyoishia kuwa na wachezaji tisa

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wenyeji Canada wamewadhalilisha wenyeji wa fainali zilizopita za 2022 Qatar kwa kuwachabanga 6-0.

    Kila kipindi kilizaa magoli matatu huku Qatar wakimaliza na wachezaji tisa dimbani kutokana na wachezaji wake wawili kutolewa nje kwa kadi nyekundu.

    Mchezaji Jonathan David wa Canada anayecheza katika klabu ya Juventutus Tulin ya Italia alipachika magoli matatu na kuwa wa pili katika fainali za mwaka huu baada ya Lonel Messi kufanya vivyo hivyo dhidi ya Algeria.

    Kabla ya hapo, Uswiss iliionesha Bosnia Herzegovina kile kilichomnyoa kanga manyoya kwa kuwashushia kichapo cha mogili 4-1 huku kiungo Jonathan Manzambi anayesakata soka katika klabu ya Freiburg ya Ujerumani akiziona nyavu mara mbili.

    Soma zaidi:

  4. Kombe la Dunia 2026: Mexico yafuzu kutoka hatua ya makundi baada ya kuifunga Korea Kusini

    G

    Chanzo cha picha, Reuters

    Timu ya taifa ya Mexico imekuwa ya kwanza kufuzu hatua inayofuata ya mashindano baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1 kwa 0 dhidi ya Korea Kusini.

    Mexico, ambayo ilishinda mechi yake ya kwanza dhidi ya Afrika Kusini kwa mabao 2 kwa 0 baada ya sherehe za ufunguzi jijini Mexico City, ilipata ushindi wake wa pili Alhamisi usiku baada ya Romo kufunga bao pekee la mchezo katika dakika ya 50.

    Kwa ushindi huo, Mexico imefikisha pointi sita na kufuzu rasmi hatua inayofuata huku ikiwa bado haijaruhusu kufungwa bao lolote katika mashindano hayo.

    Korea Kusini, ambayo ilifanya mgeuko wa kuvutia na kuifunga Czechia katika mchezo wake wa kwanza, ilikuwa ikitarajia kufuzu kwa kuishinda Mexico. Hata hivyo, baada ya kipigo hicho, italazimika kuepuka angalau kushindwa katika mechi yake ya mwisho dhidi ya Afrika Kusini ili kuendelea na mashindano.

    Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Afrika Kusini na Czechia zilitoka sare na kila timu kujikusanyia pointi yake ya kwanza. Matokeo hayo yanamaanisha kuwa timu zote mbili zinapaswa kushinda mechi zao za mwisho ili kudumisha matumaini ya kufuzu.

    Kwa upande wa bara la Asia, Alhamisi haikuwa siku nzuri. Mbali na Korea Kusini kupoteza dhidi ya wenyeji Mexico, Qatar ilikumbana na kipigo kizito cha mabao 6 kwa 0 dhidi ya Canada, hali iliyozifanya timu za Asia kushindwa kuhimili ushindani wa wenyeji na wapinzani wao.

    Soma zaidi:

  5. Iran yatafuta maridhiano na majirani zake wa Ghuba baada ya makubaliano na Marekani

    H

    Chanzo cha picha, EPA

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Kuwait, Abdullah Ali Al Yahya, akisisitiza umuhimu wa mazungumzo kati ya Iran na mataifa ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi ili kupunguza kile alichokiita “kutokuelewana” na kuimarisha uhusiano wa kikanda.

    Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Alhamisi, Araghchi pia alieleza matumaini yake kwamba makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yatachangia kurejesha amani na utulivu katika eneo hilo.

    Soma zaidi:

  6. Trump: Natarajia makubaliano ya kusitisha mapigano yaheshimiwe katika pande zote, ikiwemo Lebanon

    d

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Siku moja baada ya kutiwa saini kwa makubaliano kati ya Iran na Marekani, Rais wa Marekani Donald Trump amesema anatarajia usitishaji mapigano kuheshimiwa katika maeneo yote ya mzozo, ikiwemo Lebanon.

    Wakati nchini Marekani mjadala mkubwa umejikita katika masharti ya kiuchumi na vipengele vinavyohusu mpango wa nyuklia wa Iran, mjini Tehran mjadala umeelekezwa zaidi kwenye hatma ya Mlango Bahari wa Hormuz na kuendelea kuwepo kwa majeshi ya Israel nchini Lebanon. Masuala hayo yamevutia kwa kiasi kikubwa viongozi wa Iran, hususan wahafidhina wenye msimamo mkali.

    Alhamisi, katika ujumbe uliohusishwa na Mojtaba Khamenei, anayeelezwa kama kiongozi mpya wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, alisema alikuwa na mtazamo tofauti kuhusu makubaliano hayo, lakini alikubali yaendelee na sasa anasubiri kuona jinsi yatakavyotekelezwa.

    Wakati huo huo nchini Uswisi, ambako mazungumzo zaidi yanatarajiwa kufanyika, usalama umeimarishwa katika eneo litakalowakutanisha Makamu wa Rais wa Marekani J.D. Vance na Spika wa Bunge la Iran Mohammad Baqer Qalibaf siku ya Ijumaa.

    Soma zaidi:

  7. Hujambo na karibu kwa matangazo yetu ya moja kwa moja ya tarehe 19 Juni 2026.