Mwanaharakati wa India aliyegoma kula kwa siku 20 apelekwa hospitalini kwa nguvu

Chanzo cha picha, Getty Images
Mwanaharakati na msomi wa India Sonam Wangchuk, ambaye alikuwa kwenye mgomo wa kula kwa siku 20 zilizopita huko Delhi, ameondolewa kwa nguvu kutoka eneo lake la maandamano.
Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 59 alikuwa akiandamana kuunga mkono harakati za kejeli mtandaoni zinazoitwa Cockroach Janta Party (CJP) zinazotaka mageuzi ya kielimu. Waandamanaji walikuwa wamepanga maandamano hadi bunge la India siku ya Jumatatu.
Wangchuk alikuwa amegoma kula chakula wakati wa kiangazi chenye joto kali, huku akila chumvi na maji tu. Alikuwa amepunguza uzito zaidi ya kilo 9 na alikuwa na maumivu makali.
Mwanzilishi wa CJP Abhijeet Dipke sasa ameanza mfungo usiojulikana badala yake. Anasema maandamano ya kuelekea bungeni yataendelea na amemtaka Waziri Mkuu Narendra Modi ajiuzulu.
Dipke aliambia BBC kwamba alikuwa ameenda nyumbani kwa rafiki yake asubuhi ili kupumzika wakati polisi walipofika na kukataa kumruhusu aondoke.
Video kutoka kwenye tovuti ya maandamano siku ya Jumamosi zilionyesha machafuko yakizuka kabla tu ya saa 1:30 kwa saa za huko (02:00 GMT) wakati polisi kadhaa na wanajeshi walipoingia ghafla kwenye jukwaa ambalo mwanaharakati huyo alikuwa amelala. Waandamanaji waliojaribu kuwazuia walisukumwa mbali.
Walimfunika kwa mapazia ya shuka kabla ya kumtoa jukwaani. Dakika chache baadaye, ambulensi ilionekana ikiondoka kwa kasi.
Mke wa mwanaharakati huyo Gitanjali Angmo baadaye alichapisha kwenye mtandao wa X kwamba alikuwa "katika hospitali ya Safdarjung ambapo amelazwa".
Soma Zaidi:



















