Mwanangu si 'shetani' , asema mama Diddy

Chanzo cha picha, Getty Images
Mama yake Sean "Diddy" Combs amesema "amesikitishwa na kuhuzunishwa sana" na tuhuma zinazotolewa dhidi ya mwanaye, zilizo za "uongo".
Mwanamuziki huyo, anayejulikana kwa vibao kama vile I'll Be Missing You, 1997 alikamatwa kwa tuhuma za ulanguzi wa ngono na ulaghai mwezi uliopita.
Kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha Manhattan baada ya kunyimwa dhamana.
Katika taarifa yake, Janice Small Combs alimtetea mwanaye, akisema kwamba ingawa "alifanya makosa siku za nyuma, kama sisi sote ambavyo tumefanya", yeye "sio mnyama ambaye wanamuonesha". "Inasikitisha kuona mwanangu akihukumiwa bila ukweli, lakini kwa simulizi iliyotengenezwa kwa uwongo," aliandika.
Hatua hiyo Ilikuja siku tano baada ya kufichuliwa kwamba Bw Combs anaweza kukabiliwa na mashtaka kutoka kwa washitaki zaidi ya 100, wanaume na wanawake, kwa madai ya unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji. Wakili wa nyota huyo amekanusha mashtaka hayo na mengine yote ya awali, akiyataja kuwa ya "uongo na kashfa".
Amekabiliwa na kesi kadhaa tangu mwaka jana, wakati mpenzi wake wa zamani Cassie Ventura alipomshtaki kwa ubakaji na unyanyasaji.
Bw.Combs alikanusha madai hayo, na kesi hiyo ilitatuliwa nje ya mahakama siku moja baada ya kuwasilishwa.
Unaweza kusoma;





