Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Hezbollah yasema 'ina imani' inaweza kuzuia uvamizi wa Israel

Katika taarifa mpya ya kuadhimisha mwaka mmoja tangu mashambulizi ya Oktoba 7 ya Hamas, Hezbollah inasema ina "ujasiri" katika uwezo wake wa "kuzuia uvamizi wa [Israel]", na imeapa kuendelea kupigana.

Muhtasari

  • Hezbollah yasema 'ina imani' inaweza kuzuia uvamizi wa Israel
  • Mwanamume akumbuka maisha 'mazuri' kabla ya vita kuua jamaa wake Gaza
  • Makumbusho yafanyika mwaka mmoja tangu kutokea kwa shambulizi la Hamas
  • 'Mwanaume aliyetekwa nyara Oktoba 7 auawa'
  • Jeshi la Israel lashambulia maeneo ya Hamas kote Ukanda wa Gaza
  • Mwanajeshi wa Israel auawa kwenye mpaka wa Lebanon
  • Mlipuko waua Wachina wawili karibu na uwanja wa ndege wa Karachi, Pakistan
  • Mwanaharakati wa upinzani wa Urusi aliuawa akipigania Ukraine
  • ‘Binti yangu mateka wa Uingereza-Israel amesahaulika’ - mama

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Mwanangu si 'shetani' , asema mama Diddy

    Mama yake Sean "Diddy" Combs amesema "amesikitishwa na kuhuzunishwa sana" na tuhuma zinazotolewa dhidi ya mwanaye, zilizo za "uongo".

    Mwanamuziki huyo, anayejulikana kwa vibao kama vile I'll Be Missing You, 1997 alikamatwa kwa tuhuma za ulanguzi wa ngono na ulaghai mwezi uliopita.

    Kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha Manhattan baada ya kunyimwa dhamana.

    Katika taarifa yake, Janice Small Combs alimtetea mwanaye, akisema kwamba ingawa "alifanya makosa siku za nyuma, kama sisi sote ambavyo tumefanya", yeye "sio mnyama ambaye wanamuonesha". "Inasikitisha kuona mwanangu akihukumiwa bila ukweli, lakini kwa simulizi iliyotengenezwa kwa uwongo," aliandika.

    Hatua hiyo Ilikuja siku tano baada ya kufichuliwa kwamba Bw Combs anaweza kukabiliwa na mashtaka kutoka kwa washitaki zaidi ya 100, wanaume na wanawake, kwa madai ya unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji. Wakili wa nyota huyo amekanusha mashtaka hayo na mengine yote ya awali, akiyataja kuwa ya "uongo na kashfa".

    Amekabiliwa na kesi kadhaa tangu mwaka jana, wakati mpenzi wake wa zamani Cassie Ventura alipomshtaki kwa ubakaji na unyanyasaji.

    Bw.Combs alikanusha madai hayo, na kesi hiyo ilitatuliwa nje ya mahakama siku moja baada ya kuwasilishwa.

    Unaweza kusoma;

  2. Hezbollah yasema 'ina imani' inaweza kuzuia uvamizi wa Israel

    Katika taarifa mpya ya kuadhimisha mwaka mmoja tangu mashambulizi ya Oktoba 7 ya Hamas, Hezbollah inasema ina "ujasiri" katika uwezo wake wa "kuzuia uvamizi wa [Israel]", na imeapa kuendelea kupigana.

    Kundi hilo lenye makao yake makuu Lebanon linashirikiana na Hamas, na yote yanaungwa mkono na kufadhiliwa na Iran.

    Hezbollah inayaelezea matukio ya tarehe 7 Oktoba kama "ya kishujaa", ikisema yatakuwa na athari za "kihistoria" katika eneo hilo.

    "Hakuna mahali" kwa Israel huko, inasema, na "lazima iondolewe, haijalishi itachukua muda gani".

    Hezbollah pia inalaumu "Marekani na washirika wake" kwa ghasia huko Gaza na Lebanon iliyofuata shambulio la Hamas la Oktoba 7, wakisema "wanawajibika kikamilifu".

    Soma zaidi:

  3. Makumbusho yafanyika mwaka mmoja tangu kutokea kwa shambulizi la Hamas

    Asubuhi ya leo, watu wamerejea kwenye eneo kulikofanyika shambulio wakati tamasha lilikuwa likiendelea la Supernova huko Re'im, kusini mwa Israel, ambapo zaidi ya watu 350 waliuawa na Hamas mwaka mmoja uliopita leo.

    Wakati huohuo, jamaa walishikilia picha za wapendwa wao waliokuwa kwenye tamasha hilo.

    Wengi katika sherehe hiyo wamevalia fulana zenye picha za wapendwa wao

  4. Mwanaume aliyetekwa nyara Oktoba 7 auawa - Jukwaa la Familia Zilizotoweka limesema

    Idan Shtivi, mmoja wa mateka waliochukuliwa na Hamas kutoka tamasha la muziki la Supernova tarehe 7 Oktoba mwaka jana, ameuawa, Jukwaa la Mateka na Familia Zilizotoweka linasema.

    Kundi hilo ambalo linalenga kuwarejesha waliotekwa nyara nchini Israel, linasema kijana huyo mwenye umri wa miaka 28 "alijulikana kwa kujitolea kwa ajili ya wale walio karibu naye".

    Jukwaa hilo limeongeza kuwa wakati shambulio hilo lilipoanza, Shtivi aliamua "kujitolea" kusaidia watu wawili wasiojulikana kutoroka kutoka kwa eneo la tukio, lakini gari lao lilishambuliwa njiani.

    Miili ya watu hao wawili ilipatikana.

    Hamas iliteka nyara watu 251 wakati wa mashambulizi ya Oktoba 7, kulingana na takwimu za Israel.

    Kabla ya kifo cha Shtivi kutangazwa, 117 kati ya wale waliochukuliwa mateka walikuwa wameachiliwa, 37 walithibitishwa kufariki, na 97 hawajulikani waliko.

    Soma zaidi:

  5. Mlipuko waua Wachina wawili karibu na uwanja wa ndege wa Karachi, Pakistan

    Raia wawili wa China wameuawa na takriban watu kumi kujeruhiwa baada ya mlipuko kutokea karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jinnah mjini Karachi, Pakistan.

    Ubalozi wa China nchini Pakistan ulisema kulikuwa na "baadhi ya majeruhi wa eneo hilo" katika kile ulichokitaja kama "shambulio la kigaidi", ingawa jumla ya vifo bado haijulikani wazi.

    Ubalozi umeongeza kuwa mlipuko huo ulilenga msafara wa wahandisi wa China wanaofanya kazi katika mradi wa umeme katika mkoa wa Sindh nchini humo.

    Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu, kundi hilo la wanamgambo lilisema "lililenga msafara wa ngazi ya juu wa wahandisi na wawekezaji wa China" unaowasili kutoka uwanja wa ndege wa Karachi.

    Shambulio hilo lilitekelezwa kwa kutumia "kifaa cha vilipuzi kinachobebwa kwenye gari", Reuters ilinukuu BLA ikisema.

    Mlipuko ulitokea mwendo wa 23:00 saa za eneo. Ubalozi wa China ulisema kuwa wahandisi hao walikuwa sehemu ya kampuni inayofadhiliwa na China ya Port Qasim Power Generation Co Ltd, ambayo inalenga kujenga mitambo miwili ya kuzalisha umeme wa makaa ya mawe huko Port Qasim, karibu na Karachi.

    Kiwanda hicho ni sehemu ya ukanda wa uchumi wa China na Pakistan, ambao pia unafadhili miradi kadhaa ya miundombinu na nishati katika jimbo la Balochistan nchini Pakistan, ambalo lina utajiri mkubwa wa maliasili, ikiwa ni pamoja na gesi na madini.

    Jeshi la Balochistan (BLA), ambalo katika miaka ya hivi karibuni limefanya mashambulizi dhidi ya raia wa China wanaohusika na miradi, limedai kuhusika na shambulio hilo.

    Mara kwa mara kundi hilo limekuwa likilenga raia wa China katika eneo hilo, likidai wakaazi wa kabila la Baloch hawakuwa wakipata mgao wao wa mali inayotokana na wawekezaji wa kigeni.

    Pia unaweza kusoma:

  6. 'Binti yangu aliyetekwa na Hamas amesahaulika' - Mama

    Mama wa mateka pekee raia wa Uingereza na Israel ambaye bado anashikiliwa na Hamas huko Gaza ameuliza kwa nini Uingereza "haipiganii kwa kila namna kuhakikisha kuachiliwa kwake".

    Emily Damari, 28, alipigwa risasi na kuchukuliwa kutoka eneo la kibbutz la Israel na kuvukishwa mpaka hadi Gaza mnamo 7 Oktoba.

    Akizungumza katika hafla ya kumbukumbu ya London kuashiria mashambulizi mwaka mmoja uliopita, mama yake Mandy Damari alisema "shida ya bintiye inaonekana kuwa imesahauliwa".

    Waziri Mkuu Sir Keir Starmer alisema katika taarifa kwamba Uingereza "bila shaka ni lazima isimame na jumuiya ya Wayahudi".

    Binti huyo mwenye uraia mara mbili ni miongoni mwa mateka 97 ambao bado hawajulikani waliko.

    Akiongea kwenye hafla ya ukumbusho ya Hyde Park, mama yake alisema: "[Emily] ni binti wa nchi zote mbili, lakini hakuna mtu anayetaja ukweli kwamba bado kuna mateka wa kike wa Uingereza anayeshikiliwa na Hamas kwa mwaka mmoja sasa. Na mimi wakati mwingine hushangaa kama watu wanajua kuna mwanamke wa Uingereza huko Gaza.

    "Fikiria, kama Emily angekuwa binti yako. Jaribu kuwazia anachopitia.

    "Tangu tarehe 7 Oktoba mwaka jana, amekuwa akishikiliwa na magaidi wa Hamas katika mahandaki ya Gaza, mita 20 au zaidi chini ya ardhi akiwa amefungiwa, kuteswa, kutengwa, kutoweza kula, kuzungumza au hata kusonga bila ruhusa ya mtu mwingine.”

    Soma zaidi:

  7. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja ikiwa ni tarehe 07/10/2024