Rais Ruto wa Kenya apunguza bei ya mafuta ya dizeli kwa shillingi 10
Rais wa Kenya William Ruto, ametangaza kupunguza bei ya mafuta ya dizeli kwa shillingi kumi zaidi, katika mabadiliko ya bei ya mafuta yatakayo tangazwa mwezi Juni na Julai.
Iwapo pendekezo la Rais litatekelezwa, bei ya mafuta ya dizeli itashuka na kufikia shillingi 222.86 au dola 1.72 kutoka shillingi 242.92 (dola 1.87)
Awali serikali ilikuwa imetangaza kupunguza bei ya mafuta ya dizeli kwa shillingi kumi, huku rais Ruto akilaumu vita eneo la Mashariki ya Kati, kuwa vimechochea kupanda kwa bei ya mafuta.
Rais Ruto alitoa taarifa hiyo baada ya kukutana na viongozi wa vyama na miungano ya magari ya uchukuzi, ambao walifanya mgomo mapema wiki hii wakilalamikia kupanda kwa bei ya mafuta.
Viongozi wa muungano wa wamiliki magari ya uchukuzi maarafu matatu, wametangaza kuwa wamesitisha mgomo wao kabisa, baada ya kuafikiana na serikali kufanya mageuzi katika bei ya mafuta na kubadilishwa kwa sera zinazoiendesha sekta hiyo.
Pia unaweza kusoma: