Nasa yazindua hatua zinazofuata za kujenga kituo cha kudumu mwezini
Nasa imetoa maelezo ya vifaa inayopania kupeleka anga za juu ikiwa ni pamoja na roboti, ndege zisizo na rubani na magari ambayo kama sehemu ya mipango ya Marekani ya kujenga kituo cha anga mwezini.
Kampuni ya anga ya juu ya mwanzilishi wa Amazon Jeff Bezos ya Blue Origin ni mojawapo ya makampuni kadhaa yaliyochaguliwa kujenga mashine hizo.
Marekani inataka kuwarejesha Wamarekani kwenye Mwezi kabla ya Rais Donald Trump kuondoka madarakani mwaka 2029.
Lakini Nasa inashindana na China kurudisha wanadamu mwezini, kumaanisha shirika hilo la anga liko chini ya shinikizo la kushinda mbio mpya za anga.
China inaendelea mbele na mipango yake ya kuwapeleka wanadamu Mwezini ifikapo 2030.
Siku ya Jumatatu ilizindua chombo chake cha anga za juu cha Shenzhou-23, na kutuma wafanyakazi wa wanaanga kwenye kituo cha anga za juu cha Tiangong nchini humo.
Mnamo Machi, Nasa ilitangaza mpango wa dola bilioni 20 wa kujenga kituo cha kudumu itakayoendeshwa na nguvu ya nyuklia na nishati ya jua kwenye ncha ya kusini ya Mwezi ifikapo 2032.
Msimamizi wa Nasa Jared Isaacman alisema Jumanne kwamba matangazo hayo yanamaanisha Marekani "haitaachana tena na harakati zake mwezini".
Soma zaidi: