Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Boeing iliitaka Pentagon iiruhusu kuipelekea Ukraine makombora ya GLSDB - Silaha hii ni gani?
Pentagon inafikiria kusafirisha makombora mapya ya masafa marefu hadi Ukraine, Reuters inaripoti.
Kulingana na shirika hilo la habari, Shirika la Boeing limeambia Wizara ya Ulinzi ya Marekani kwamba liko tayari kusafirisha risasi za bomu hilo lililozinduliwa chini ya ardhi (GLSDB) zenye uwezo wa kukrika hadi kilomita 150 kwa Waukraine.
Hii itairuhusu Ukraine kufikia malengo ya ndani ya Urusi, ambayo bado hayajafikiwi.
Vikosi vya Ukraine tayari vimefanikiwa kutumia mfumo wa roketi za GMLRS yenye usahihi wa hali ya juu katika vita, kulenga shabaha kwa umbali wa zaidi ya kilomita 70.
Lakini, kama gazeti la New York Times la Marekani lilivyoripoti hivi karibuni, nchi za Magharibi zilianza kukabiliwa uhaba wa sila za kutuma Ukraine.kilomita 70.
GLSDB, ambayo Reuters inaandika juu yake, inaweza kuchukua nafasi ya GMLRS kwa ufanisi, kwa kuwa ni ya bei nafuu na ina uwezo mkubwa wa kufikia malengo ya shabaha.
GLSDB ni muendelezo wa pamoja kati ya Boeing na Saab Group. Ni bomu la GBU-39 linaloongozwa kwa usahihi lililoimarishwa kwa uzinduzi wa ardhini.
Kwa hili, sehemu ya roketi ya risasi ya M26, iliyotengenezwa kwa vizindua vya M270 MLRS na M142 HIMARS, hutumiwa.
Silaha ya zamani
M26 ni kombora la zamani. Iliundwa mwishoni mwa miaka ya 1970, na utayarishaji ulianza mnamo 1980. Roketi hizi zisizo na mwongozo hutumia mabomu ya nyuklia.
Tangu 1980, zaidi ya makombora elfu 400 ya M26 ya yaliyoimarishwa yameundwa. Hata hivyo, kama sehemu ya kampeni ya kupunguza mabomu ya vishada, Jeshi la Marekani limeondoa sehemu kubwa ya makombotra ya M26.
Data kamili kuhusu ni makombora mangapi ya M26 yaliyosalia Marekani na katika nchi zilizopewa haipatikani katika vyanzo huria.
Katika tovuti ya Harakati ya Kimataifa ya Kupiga Marufuku Makombora ya kivita, katika ukurasa wa programu inayofuatilia uharibifu mabomu hayo, inasema kwamba mwaka wa 2004 makombora 369,576 ya M26 yenye vichwa vya nyuklia yalisalia kwenye ghala za kijeshi za Marekani.
Kwa mujibu wa Human Rights Watch, makombora hayo yalitolewa kwa Bahrain, Misri, Ufaransa, Ujerumani, Ugiriki, Israel, Italia, Japan, Korea Kusini, Uturuki, Uingereza na Uholanzi.
Tovuti ya Jeshi la Marekani ya mwaka wa 2013 iliyochapisha kuhusu kuharibiwa kwa silaha hizi ilisema kwamba teknolojia hiyo ilihusu vichwa vya makombora, na haikutaja kuharibiwa kwa wa sehemu ya roketi. Mojawapo ya malengo ya maendeleo ya GLSDB ilikuwa kutumia sehemu za kombora za M26 zilizokataliwa.
Mrengo wa kulia
Boeing na Lockheed Martin walianza kutengeneza bomu la GBU-39 mwanzoni mwa miaka ya 2000.
Wazo lilikuwa kuunda bomu ambalo lingefidia salaha ndogo inayofanya kazi kwa usahihi wa hali ya juu.
Kichwa cha kombora hilo kimeundwa ili kuharibu malengo yaliyoimarishwa, na inaweza kupenya hadi mita moja ya saruji iliyoimarishwa.
Bomu hilo ambalo lilianza kutumika mwaka 2006, linatumia mfumo wa satelaiti wa kuelekeza shabaha.
Baada ya kurushwa kutoka kwa ndege, kombora hilo hufungua bawa la kukunja, ambalo huongeza ukubwa wa ndege. GLSDB ndio toleo la msingi la bomu hili.
Gazeti la New York Times liliandika kwamba Marekani na nchi nyingine za NATO zinapata shida kupata akiba ya usambazaji wa silaha mpya kwa Ukraine. Kwanza kabisa, hii inahusu makombora ya mizinga, hata hivyo, kwa kuzingatia mpango wa Shirika la Boeing, Marekani inatafuta njia mbadala ya makombora ya usahihi wa hali ya juu kwa ajili ya mitambo ya HIMARS na MLRS.
Ukraine imekuwa ikiomba Marekani kwa makombora yenye nguvu zaidi ya MGM-140 ATACMS kwa ajili ya HIMARS na MLRS kwa miezi kadhaa sasa. Umbali wa makombora hayo ni kilomita 300. Hata hivyo, makombora haya bado hayajakabidhiwa kwa Waukraine, na mipango ya kusafirishwa kwa haijaripotiwa katika vyanzo vya wazi.
Hakuna taarifa kuhusu gharama halisi ya GLSDB katika vyanzo wazi, hata hivyo, kulingana na data iliyochapishwa kwenye tovuti ya Jeshi la anga la Marekani, itagharimu zaidi ya dola elfu 40.
Bomu la angani la GBU-39 ndio sehemu kuu ya kombora la GLSDB. Sehemu ya kombora kutoka M26 inaweza kuchukuliwa kutoka kwa uhifadhi. Ipasavyo, gharama ya vitengo vya kukusanya bidhaa na kazi lazima iongezwe kwa bei hii. Gharama ya roketi ya GMLRS, kulingana na makadirio mbalimbali, ni kutoka dola elfu 100 hadi dola elfu 160.
Kichwa cha vita cha GMLRS kina uzito wa kilo 90, ambayo ni sawa na uzito wa GLSDB (yenye uzito - kilo 93).
Wakati huo huo, wataalam wengi walibaini kuwa roketi ya GMLRS haina nguvu ya kutosha kuharibu vitu vya kudumu, kama vile madaraja.
Mchanganyiko wa gharama, anuwai na usahihi wa hali ya juu wa GLSDB hufanya toleo hili liwe la faida kwa usafirishaji kwenda Ukraine.
Hata hivyo, haijulikani ni mabomu mangapi ya kuongozwa yaliundwa na ni kiasi gani Marekani inaweza kumudu kujitolea katika utengenezaji wa makombora hayo.