Kombe la Dunia 2018: Mwandishi wa kike apigwa busu kwa lazima akitangaza

A female reporter is kissed, by a fan, clearly looking uncomfortable, holding a DW mic

Chanzo cha picha, DW Espanol

Maelezo ya picha, "Ni kuvuka mipaka," Gonzalez Theran alisema kuhusu tukio hilo.
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 1

Mwanahabari mmoja wa kike amepigwa busu kwa lazima na kunyanyaswa akifanya ripoti kuhusu Kombe la Dunia.

Mtangazaji huyo raia wa Colombia Julieth Gonzalez Theran alikuwa akitangazia moja kwa moja shirika la Habari la DW Espanol .

Tukio hilo limetokea mjini Moscow wakati mwanaume mmoja alipojitokeza na kumshika maziwa kabla ya kumpiga busu.

Ingawa Julieth aliendelea na kazi yake, alililizungumzia tukio hilo baadaye.

"Sikustahili kutendewa vile," Gonzalez Theran alisema. "Tuko na thamani na weledi pia."

Amemueleza mwajiri wake, Deutsche Welle, alikuwa eneo la tukio kwa muda wa saa mbili akijiandaa.

"Tulipoanza kupeperusha matangazo, shabiki mmoja alichukua fursa hiyo," aliongeza. "Lakini baadaye, nilipoangalia kuona iwapo alikuwa eneo lile, sikumuona."

Kisa hicho kilitokea juma lililopita mjini Saransk kabla ya mechi kati ya Russia na Saudi Arabia.

DW iliweka kanda ya video ya tukio hilo kwenye mtandano na kushutumu tukio hilo kuwa "uvamizi" na "unyanyasaji".

Hata hivyo wengine wameita tukio hilo kuwa la kawaida.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

"Kulingana na mimi, sio kawaida," Gonzalez Theran alifafanua. "Kuna watazamaji wa kukushabikia kwa ustaarabu, hili lilivuka mpaka."

"Si mzaha," Mtangazaji wa DW Cristina Cubas aliandika kwenye twitter. "Si busu. Ni uvamizi."

Unyanyasaji wa watangazaji wa kike sio jambo geni kwneye michezo.

Maelezo ya video, Hassanati Swaleh: Brazil iko kwenye damu yangu

Mwaka uliopita mchezaji wa tenisi Maxime Hamou alipigwa maruuku kutoka kombe la French Open baada ya kumbusu mtangazaji wa kike kwa lazima kwenye mahojiano ya moja kwa moja.

"Iwapo singekuwa hewani, ningempiga ngumi ," alisema mtangazaji huyo, Maly Thomas, baada ya tukio.