Tetesi za soka Jumanne 09.06.2026

Chanzo cha picha, Getty Images
Tottenham wanaendelea na mazungumzo kuhusu dili la takribani £60m kwa ajili ya winga wa Manchester City, Mbrazili Savinho, mwenye umri wa miaka 22. (Mail)
Manchester United bado wana nia ya kumsajili Elliot Anderson, huku viongozi wa klabu wakiwa na matumaini ya kuipiku Manchester City katika mbio za kumnasa kiungo huyo Muingereza mwenye umri wa miaka 23, anayekadiriwa kuwa na thamani ya takribani £100m na Nottingham Forest. (Guardian)
Inasemekana Anderson ameonesha nia ya kujiunga na Manchester City badala ya Manchester United. (Talksport)
Atletico Madrid na FC Barcelona zipo katika nafasi nzuri ya kumsajili beki wa Chelsea Marc Cucurella, 26, ambaye anataka mabadiliko baada ya miaka minne Stamford Bridge. (Marca)
Newcastle United itamfuatilia kiungo wa Monaco, Lamine Camara, 22, endapo Sandro Tonali au Joe Willock wataondoka St James’ Park msimu huu wa joto. (Telegraph)
Macho ya skauti wa Manchester United yalimfuatilia mshambuliaji chipukizi wa Inter Milan, Pio Esposito, 20, alipokuwa akiichezea Italia dhidi ya Ugiriki katika mechi ya kirafiki. (Teamtalk)
Mshambuliaji wa Ufaransa wa Paris Saint-Germain, Randal Kolo Muani, 27, ambaye alicheza kwa mkopo Tottenham msimu uliopita, anataka kujiunga na Juventus. (Tuttosport)
Manchester City wanafikiria kumsajili winga wa Real Madrid Rodrygo, 25, na Iliman Ndiaye wa Everton na Senegal, 26. (Mail)
Beki wa kati Mreno Gonçalo Inácio wa Sporting yuko kwenye orodha ya Liverpool FC kama mbadala wa Ibrahima Konaté anayeondoka. (CaughtOffside)
Atalanta BC wanafanya mazungumzo na Nottingham Forest kumrudisha beki Nicolò Savona, 23, Serie A. (Goal)
AC Milan wanatarajiwa kufanya duru ya pili ya mazungumzo na kocha wa zamani wa Crystal Palace Oliver Glasner kuwa meneja mpya. (Calciomercato)
















