Moja kwa moja, Marekani yamwekea vikwazo Kabila kwa tuhuma za kuunga mkono makundi ya waasi DR Congo

Washington inadai Kabila alitoa msaada wa kifedha kwa AFC, kuhamasisha wanajeshi kuasi kutoka jeshi la Congo, na kupanga mashambulizi dhidi ya vikosi vya serikali.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Kujenga upya silaha za Marekani baada ya vita na Iran itachukua miezi hadi miaka – Waziri wa ulinzi

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Maelezo ya picha, Waziri wa Ulinzi nchini Marekani Pete Hegseth

    Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegsett ametangaza katika mkutano na wajumbe wa Congress kwamba kujenga upya hifadhi za silaha za Marekani, ambazo zimepungua kufuatia vita na Iran na migogoro mingine ya kijeshi katika miaka ya hivi karibuni, inaweza kuchukua "miezi hadi miaka," kulingana na aina ya vifaa.

    Seneta Mark Kelly wa Arizona alimuuliza Bw. Hegsett kwenye sakafu ya Seneti itachukua muda gani kuchukua nafasi ya hifadhi.

    "Mashambulizi mengi haya yanatumia silaha zetu bora, na tunatumia nyingi, pamoja na viingilia.

    Huwezi kuzalisha silaha hizi mara moja," alisema.

    Seneta Kelly aliongeza kuwa ombi la bajeti lililowasilishwa linaonyesha kuwa Idara ya Ulinzi pia ina ushahidi wa suala hili na kutaka ratiba maalum ya kubadilisha mifumo hii.

    "Hilo ndilo swali linalohitaji kuulizwa," Bw. Hegst alijibu, akisisitiza kwamba kujenga upya hifadhi kunaweza kuchukua kutoka kwa miezi michache hadi miaka michache, kulingana na aina ya mfumo wa silaha.

    Pia unaweza kusoma:

  2. Mshukiwa ashtakiwa kwa jaribio la mauaji baada ya Wayahudi wawili kuchomwa kisu Uingereza

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Essa Suleiman amefunguliwa mashtaka ya jaribio la mauaji baada ya wanaume wawili wa Kiyahudi kuchomwa kisu Golders Green, kaskazini mwa London, Polisi wa Metropolitan wamesema.

    Kijana huyo mwenye umri wa miaka 45 ameshtakiwa kwa makosa mawili ya kujaribu kuua na shtaka moja la kupatikana na kifaa chenye ncha kali katika eneo la umma kuhusiana na tukio hilo la Jumatano.

    Pia ameshtakiwa kwa jaribio la mauaji kuhusiana na tukio tofauti katika mtaa wa Great Dover huko Southwark mapema siku hiyo hiyo.

    Siku ya Alhamisi, kiwango cha tishio la ugaidi nchini Uingereza kilipandishwa kufuatia shambuliwa la kisu dhdi ya wanaume wawili wa Kiyahudi.

    Serikali inasema kuwa kupandishwa kwa kiwango cha tishio hakukutokana tu na shambulio la Golders Green, bali pia kumechochewa na “ongezeko la vitisho vya kijihadi na vya mrengo mkali wa kulia.”

    Kamishna Mark Rowley atazungumza kwenye Kiamsha kinywa cha BBC asubuhi ya leo kuhusu tukio hilo. Tutakuwa tunakuletea sasisho zote za hivi punde hapa.

    Maelezo zaidi:

  3. Wanamgambo wa Mali wataka utawala wa kijeshi kuondolewa madarakani

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Wanamgambo wa Kiislamu nchini Mali wametoa wito kwa nchi hiyo kuungana ili kuiondoa serikali ya kijeshi.

    Katika taarifa ya mtandaoni, kundi la kijihadi lenye uhusiano na al-Qaeda, JNIM, lilitaka vyama vya siasa, vikosi vya jeshi, makundi ya wanaotaka kujitenga na viongozi wa kimila kuungana dhidi ya serikali.

    Hali hii inakuja wakati mzingiro mkali unaimarishwa kuzunguka mji mkuu, Bamako.

    Siku ya Jumatano, JNIM ilionya kuwa hakuna mtu atakayeruhusiwa kuingia mjini humo.

    Kuna mashaka kuhusu uimara wa serikali ya kijeshi ya Mali baada ya mashambulizi yaliyoratibiwa na wanamgambo wa kijihadi na wanaotaka kujitenga mwishoni mwa wiki yaliyosababisha jeshi kupoteza udhibiti wa maeneo kadhaa muhimu ya kimkakati.

    Soma zaidi:

  4. Tuzo ya Oscar yatoweka baada ya mshindi kuzuiwa kuingia nayo kwenye ndege

    ..

    Chanzo cha picha, Reuters

    Mshindi wa tuzo ya Oscar, Pavel Talankin alizuiwa kuingia kwenye ndege na tuzo yake ya dhahabu aliyoshinda kupitia filamu yake ya Mr Nobody Against Putin katika uwanja wa ndege wa New York - na sasa haipo.

    Talankin anasema alikuwa na Tuzo yake kwenye begi lake la mkononi kwenye ndege kuelekea Ujerumani siku ya Jumatano, lakini maafisa wa usalama wa uwanja wa ndege walimzuia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa John F Kennedy kwa sababu walisema tuzo hiyo inaweza kutumika kama silaha.

    Lakini alipotua Ujerumani, tuzo yake ya Oscar alikuwa ametoweka.

    Shirika la ndege ya Lufthansa, ambayo ilimsaidia kubeba tuzo hiyo kwenye sanduku la safari ya ndege kwa vile Talankin haikuwa na begi la kukaguliwa, ilisema timu yao inashughulikia tukio hilo kwa "haraka" ili "kupata'' tuzo hiyo.

    .

    Chanzo cha picha, Pavel Talankin

    "Tunajutia sana hali hii," shirika la ndege lilisema katika taarifa.

    "Maafisa wetu wanashughulikia suala hili kwa uangalifu wa hali ya juu, na tunafanya uchunguzi wa kina ili kuhakikisha Oscar anapatikana na kurudishwa haraka iwezekanavyo."

    BBC imewasiliana na Chuo cha Sanaa na Sayansi ya Picha na Mamlaka ya Usalama wa Usafiri nchini Marekani (TSA), inayoshughulikia usalama wa uwanja wa ndege ambayo ilimzuia Talankin kuingia kwenye ndege na tuzo yake.

  5. Kiongozi wa zamani wa Myanmar Aung San Suu Kyi ahamishiwa kifungo cha nyumbani

    Aung San Suu Kyi

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Serikali ya kijeshi ya Myanmar imesema kiongozi wa demokrasia aliyekuwa kizuizini, Aung San Suu Kyi, amehamishwa hadi kifungo cha nyumbani, na adhabu yake kupunguzwa hadi miaka kumi na nane.

    Vyombo vya habari vya serikali vimeonyesha picha ya mshindi wa Nobel Prize akizungumza na maafisa wawili waliovalia sare.

    Mwanawe, Kim Aris, aliiambia BBC kuwa ana uhakika picha iliyochapishwa haina maana kwa kuwa ina miaka minne, na hajapata uthibitisho wowote kama mama yake bado yuko hai.

    Alisema taarifa pekee inayopatikana imetoka kwenye taarifa kwa vyombo vya habari, na serikali ya kijeshi haiwezi kuaminika.

    '

    Chanzo cha picha, Myanmar state TV

    Bi. Suu Kyi alikamatwa baada ya serikali yake kupinduliwa kwa mapinduzi ya kijeshi mwaka 2021, na kufikishwa mahakamani kwa mashtaka ambayo kwa kiasi kikubwa yalitupiliwa mbali kama ya kutungwa.

    Pia unaweza kusoma:

  6. Kiwango cha tishio la ugaidi chapandishwa Uingereza baada ya shambulio la London

    .

    Chanzo cha picha, EPA

    Kiwango cha tishio la ugaidi nchini Uingereza kimepandishwa na serikali kutoka hadi kiwango cha pili cha juu zaidi - ikimaanisha kuwa shambulio la kigaidi linaonekana kuwa na uwezekano mkubwa kutokea ndani ya miezi sita ijayo.

    Serikali inasema kuwa kupandishwa kwa kiwango cha tishio hakukutokana tu na shambulio la Golders Green, bali pia kumechochewa na “ongezeko la vitisho vya kijihadi na vya mrengo mkali wa kulia.”

    Waziri Mkuu Keir Starmer amesema serikali sasa inazingatia kuanzisha hatua mpya, ikiwa ni pamoja na mamlaka makubwa zaidi ya “kufunga mashirika ya misaada yanayochochea chuki dhidi ya Wayahudi” na “kuzuia wahubiri wa chuki kuingia nchini humo”, pamoja na kuharakisha utoaji wa hukumu ya mashambulizi ya chuki dhidi ya Wayahudi “ili kuwe na kizuizi madhubuti.”

    “Serikali hii itafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kuondoa chuki hii. Tutaimarisha usalama wetu na kulinda jamii yetu ya Kiyahudi. Lakini pia ninatoa wito kwa kila mtu mwenye nia njema nchini kufungua macho yao kuona maumivu, mateso na hofu ya Wayahudi.”Starmer alisema.

    Shambulio la Jumatano ni la hivi karibuni katika msururu wa matukio yanayolenga jamii ya Wayahudi nchini Uingereza.

    Waziri wa Mambo ya Ndani Shabana Mahmood alisema kupandishwa kwa kiwango hicho “kutakuwa chanzo cha wasiwasi kwa wengi, hasa ndani ya jamii yetu ya Kiyahudi, ambao wamepitia mengi.”

    Mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na ugaidi jijini London aliwaambia waandishi wa habari kuwa Uingereza imekuwa “ikikabiliwa na tishio la ugaidi linaloongezeka taratibu kwa muda fulani.”

    Essa Suleiman, mwenye umri wa miaka 45, bado yuko chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kujaribu kuwaua Shloime Rand na Moshe Shine katika shambulio la Jumatano.

    Maelezo zaidi:

  7. Marekani yamwekea vikwazo Kabila kwa tuhuma za kuunga mkono makundi ya waasi DR Congo

    Kabila

    Chanzo cha picha, Reuters

    Marekani imemwekea vikwazo vikubwa Rais wa zamani wa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Joseph Kabila, ikimtuhumu kuyaunga mkono makundi ya waasi ya M23 na AFC.

    Washington inadai Kabila alitoa msaada wa kifedha kwa AFC, alihamasisha wanajeshi kuasi kutoka jeshi la Congo, na hata alijaribu mashambulizi ya kuvuka mipaka dhidi ya vikosi vya serikali.

    Maafisa wanasema lengo la Kabila lilikuwa kuyumbisha serikali iliyopo madarakani na kumuweka mgombea wa upinzani ili kurejesha ushawishi wa kisiasa.

    Chini ya uamuzi wa Wizara ya Fedha, mali zote za Kabila nchini Marekani zimezuiwa.

    Raia na kampuni za Marekani zimepigwa marufuku kufanya biashara naye, na taasisi yoyote anayodhibiti kwa asilimia 50 au zaidi pia imewekewa vikwazo.

    Benki na washirika wa kigeni wameonywa dhidi ya kushirikiana naye kwa njia isiyo ya moja kwa moja, huku ukiukaji ukibeba adhabu kali za makosa ya kiraia au jinai.

    Vikwazo hivyo vimekusudiwa si tu kuadhibu bali pia kulazimisha mabadiliko ya tabia, vikionesha utayari wa Washington kulenga viongozi wa zamani wanaotuhumiwa kuchochea migogoro.BBC ilitafuta maoni kutoka jopo la mawasiliano la Kabila lakini bado haijapata majibu.

    Septemba, 2025, Mahakama ya Kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu kifo bila kuwepo mahakamani kwa kosa la uhaini, uhalifu wa kivita na kushirikiana na M23, aliporejea nchini kutoka uhamishoni mapema mwaka huo.

    Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent alisema hatua hizo zinaimarisha makubaliano ya amani na Ustawi ya Washington, zilizosainiwa Disemba, 2025 kati ya DRC na Rwanda.

    Aliongeza kuwa Rais Donald Trump ameweka wazi kwamba wale wanaosambaza machafuko watawajibishwa.

    Vikwazo hivyo vinafuatia hatua za awali za Marekani dhidi ya jeshi la Rwanda Machi, 2026, iliyotuhumiwa kuunga mkono kutekwa kwa miji ya Goma na Bukavu na kundi la M23.

    Kigali imekanusha madai hayo, ikisisitiza kuwa hatua zake zilikuwa za kujilinda.

    Kabila, ambaye alitawala DRC kuanzia mwaka 2001 hadi alipoondoka madarakani 2019, alisimamia makabidhiano ya kwanza ya madaraka kwa amani tangu uhuru wa nchi hiyo mwaka 1960.

    Soma zaidi:

  8. Karibu katika matangazo ya moja kwa moja.