Mahakama yakataa kumuachia kwa dhamana wakili wa upinzani Uganda

Chanzo cha picha, Reuters
Mahakama nchini Uganda imekataa kumuachia kwa dhamana wakili wa upinzani anayekabiliwa na mashitaka ya kujihusisha na vitendo vya uhaini.
Hayo yanajiri baada ya Mkuu wa Majeshi Uganda ambaye pia ni mwana wa Rais Yower Museveni kujigamba kuwa alimteka.
Erias Lukwago mwanasiasa na mwanasheria alifikishwa mahakamani wiki iliyopita akishitakiwa kwa kufeli kuripoti njama inayohusishwa na uhaini, waendesha mashitaka wakidai ilipangwa katika taifa jirani la Kenya kati ya 2021-2024, upande wa mashtaka ulisema.
Eric Lukwago ambaye ni wakili na mwanasiasa mashuhuri nchini Uganda, anakabiliwa na hukumu ya kifungo cha maisha gerezani ikiwa atapatikana na hatia.
Lukwago ni wakili wa mmoja wa wapinzani wakuu wa rais Yoweri Museveni. Kizza Besigye, ambaye yuko gerezani kutokana na mashtaka ya uhaini, tangu alipokamatwa nchini Kenya na kusafirishwa nyumbani mwaka wa 2024.
Mwendesha mashtaka mkuu nchini Uganda amesema kuwa kesi ya Lukwago imejumuishwa na ile ya mteja wake na kiongozi wa upinzani Kizza Besigye.
Lukawago amekanusha mashtaka dhidi yake na kuambia mahakama kuwa tangu kesi hiyo kuanza amekuwa wakili wa mshukiwa na kuhoji ni vipi wakili anaweza kuwa mshukiwa wa kesi ambayo anahusika nayo mahakamani.
Mawakili wa Lukwago wameiomba mahakama kumuachilia kwa dhamani, kwa misingi ya afya yake lakini jaji anayesikiliza kesi hiyo alikataa ombi hilo.
Jaji huyo aliagiza Lukwago kupelekewa hospitalini chini ya masaa 24 kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
Familia ya wakili huyo imesema kuwa Lukwago alikamtwa wiki iliyopita na maafisa wa ulinzi ambao hawakujitambulisha.































