Mhariri wa shirika la habari aliyedaiwa kutekwa nyara kenya apatikana
Mhariri wa shirika la habari la Standard Group, nchini Kenya Alex Kiprotich, ambaye inasemekana alitekwa nyara kando ya barabara ya Gilgil–Nakuru Jumanne usiku, alipatikana salama kwenye kichaka katika eneo la Masinga, Kaunti ya Machakos.
Mashahidi wanasema Kiprotich alionekana kutetemeka huku akiwa amejeruhiwa alipopatikana Jumatano asubuhi, saa chache baada ya tukio hilo kuripotiwa.
Alipatikana kilomita 200 kutoka mahali aliporipotiwa kutekwa nyara.
Wenzake na familia yake wanasema walipokea simu kutoka kwa nambari , walipopokea, wakamkuta Kiprotich kwenye simu.
Walikuwa wakimtafuta usiku kucha. Kiprotich alipelekwa hospitalini kwa uchunguzi.
Polisi wanasema waliarifiwa kuhusu ugunduzi huo na walikuwa wakichunguza mazingira. Sababu ya kutekwa nyara haijajulikana.