Balozi wa Marekani nchini Israel akemea makazi "haramu" ya Israel katika Ukingo wa Magharibi

Chanzo cha picha, Getty Images
Mike Huckabee, balozi wa Marekani nchini Israel, alisema kuwa raia wa Marekani wanaoishi katika eneo la makazi la Termeziya walielezea katika mkutano wa baraza la eneo hilo kuhusu nyumba zilizoharibiwa, vitisho dhidi ya watoto, pamoja na vitendo vya vurugu na vitisho vingine.
Eneo hili liko Ramallah, katika Ukingo wa Magharibi, na ni makazi ya idadi kubwa ya Wamarekani.
"Ninaamini kuwa Waisraeli wanaoishi Judea/Samaria (jina linalotumiwa na Israel kwa ajili ya eneo la Ukingo wa Magharibi linalodhibitiwa kimabavu) wana haki ya kuishi huko, na ninaunga mkono hilo, hata hivyo, si kila anayeamini katika Biblia anaunga mkono vitendo visivyo halali,"
Huckabee aliandika katika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa X. Makazi ya Waisraeli katika eneo la Ukingo wa Magharibi linalodhibitiwa kimabavu yanachukuliwa kuwa haramu kwa mujibu wa sheria za kimataifa.


