Marekani yasema meli iliyokiuka vikwazo dhidi ya Iran ililengwa kwa risasi kwenye injini

Chanzo cha picha, CENTCOM
Jeshi la Marekani limetoa maelezo zaidi kuhusu shambulio dhidi ya meli ya kubeba mafuta katika Bahari ya Oman, likisema wafanyakazi wa meli hiyo walijaribu angalau mara nne kukiuka vikwazo vinavyozuia safari kuelekea bandari za Iran kabla ya kulengwa.
Msemaji wa Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM), Tim Hawkins, ameiambia AFP kuwa wafanyakazi wa meli hiyo walionywa mara kadhaa, lakini walipuuza maagizo ya kusimama.
Alisema kuwa baada ya onyo hizo kupuuzwa, wanajeshi wa Marekani walifyatua risasi kulenga sehemu ya injini ya meli ili kuizuia kuendelea na safari.
Hawkins aliongeza kuwa meli hiyo haikuwa tena ikielekea Iran.
Awali, afisa mmoja wa Marekani aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa vikosi vya Marekani viliilenga meli ya mafuta MT Lavin baada ya kudaiwa kujaribu kukwepa vikwazo vilivyowekwa katika bandari za Iran.
Soma Pia:


























