Moja kwa moja, Trump asema Iran bado haiko tayari kufikia makubaliano na Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump amesema mazungumzo kati ya Marekani na Iran kuhusu mgogoro unaozikabili nchi hizo mbili yanaendelea, lakini Tehran bado haiko tayari kufikia makubaliano.

Ruka Video uendelee
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Mariam Mjahid

  1. Marekani yasema meli iliyokiuka vikwazo dhidi ya Iran ililengwa kwa risasi kwenye injini

    D

    Chanzo cha picha, CENTCOM

    Jeshi la Marekani limetoa maelezo zaidi kuhusu shambulio dhidi ya meli ya kubeba mafuta katika Bahari ya Oman, likisema wafanyakazi wa meli hiyo walijaribu angalau mara nne kukiuka vikwazo vinavyozuia safari kuelekea bandari za Iran kabla ya kulengwa.

    Msemaji wa Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM), Tim Hawkins, ameiambia AFP kuwa wafanyakazi wa meli hiyo walionywa mara kadhaa, lakini walipuuza maagizo ya kusimama.

    Alisema kuwa baada ya onyo hizo kupuuzwa, wanajeshi wa Marekani walifyatua risasi kulenga sehemu ya injini ya meli ili kuizuia kuendelea na safari.

    Hawkins aliongeza kuwa meli hiyo haikuwa tena ikielekea Iran.

    Awali, afisa mmoja wa Marekani aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa vikosi vya Marekani viliilenga meli ya mafuta MT Lavin baada ya kudaiwa kujaribu kukwepa vikwazo vilivyowekwa katika bandari za Iran.

    Soma Pia:

  2. Trump: Utawala wenye nguvu umeondolewa, sasa unaongozwa na kiongozi wa jinsia moja

    d

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa wakati wa uongozi wake, "utawala ambao zamani ulikuwa wa kutisha, wenye nguvu na uliokuwa ukiishambulia Marekani bila kukoma uliondolewa madarakani," ingawa hakuitaja Iran moja kwa moja.

    Akizungumza katika hafla ya Chama cha Waandishi wa Habari wa Ikulu ya White House, Trump alisema viongozi wa zamani wa utawala huo waliondolewa na sasa nchi hiyo inaongozwa na "dikteta ambaye anashiriki mahusiano ya jinsia moja anayekabiliwa na migogoro ya ndani."

    Kauli za Trump zinaonekana kuirejelea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Mojtaba Khamenei.

    Hata hivyo, hakutoa ushahidi wa kuunga mkono madai hayo, na hapo awali pia amewahi kutoa madai yanayofanana kuhusu kiongozi wa Iran.

    Unaweza kusoma;

  3. Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC Karim Khan aondolewa madarakani

    d

    Chanzo cha picha, Reuters

    Nchi wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, zimepiga kura kumwondoa Karim Khan katika wadhifa wa Mwendesha Mashtaka Mkuu kufuatia tuhuma za utovu wa nidhamu wa kingono.

    Uamuzi huo ulipitishwa Ijumaa kwa kura 82 za kuunga mkono kuondolewa kwake.

    Khan, ambaye alichaguliwa kuwa mwendesha mashtaka wa tatu wa ICC mwaka 2021, alikuwa amesimamishwa kazi mwezi uliopita wakati uchunguzi ukiendelea.

    Mnamo Juni, chombo cha usimamizi wa mahakama hiyo kilihitimisha kuwa Khan alifanya ukiukaji mkubwa wa majukumu yake na utovu mkubwa wa nidhamu kwa kuhusishwa na uhusiano wa kingono usiofaa na mfanyakazi wa ngazi ya chini wa ICC.

    Pia alidaiwa kujaribu kumzuia mfanyakazi huyo kuwasilisha malalamiko dhidi yake.

    Hata hivyo, Khan amekanusha mara kwa mara tuhuma zote zinazomkabili.

    Mawakili wake wameeleza kuwa kusimamishwa kwake kulikuwa kinyume cha sheria, hakukufuata taratibu za haki na hakukuwa na ushahidi wa kutosha kuunga mkono madai hayo.

    Kuondolewa kwa Khan kunakuja wakati ICC ikikabiliwa na changamoto kubwa zinazotishia mustakabali wake.

    Uchunguzi dhidi yake umeiweka mahakama hiyo chini ya uangalizi mkali, umeongeza migawanyiko ya ndani na umeendelea sambamba na kile kinachoelezwa kuwa juhudi zisizo za kawaida za kuidhoofisha au hata kuivunja mahakama hiyo.

    Wafuasi wa ICC wanaonya kuwa mgogoro huo unaweza kuidhoofisha mahakama hiyo na kupunguza uwezo wake wa kushughulikia uhalifu mkubwa wa kimataifa, ikiwemo uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.

    Soma Pia:

  4. Ujumbe wa Oman wawasili Iran kujadili kuhusu mgogoro wa Mlango wa Hormuz

    d

    Chanzo cha picha, Indian Navy

    Ujumbe kutoka Oman umewasili mjini Tehran kwa mazungumzo yanayohusu usimamizi wa usafiri wa meli katika Mlango wa Hormuz, kwa mujibu wa Shirika rasmi la Habari la Iran, IRNA.

    IRNA ilisema lengo la ziara hiyo ni “kuandaa utaratibu unaofaa wa kusimamia harakati za meli katika Mlango wa Hormuz.”

    Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, alifanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Oman, Badr al Busaidi, Ijumaa jioni.

    Hata hivyo, maelezo ya mazungumzo hayo hayajawekwa wazi.

    Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Iran inalenga kuratibu kwa karibu na Oman kuhusu masuala yanayohusu Mlango wa Hormuz, ambao ni njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta na bidhaa duniani.

    Ziara ya ujumbe wa Oman mjini Tehran inafanyika wakati vita kati ya Marekani na Iran vikiendelea, huku kukiwa na juhudi mpya za kufufua mazungumzo kati ya mataifa hayo mawili.

    Soma Pia:

  5. Harry Kane afanya mazungumzo ya kuongeza mkataba Bayern Munich

    d

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Nahodha wa England, Harry Kane, yuko katika mazungumzo na Bayern Munich kuhusu kuongeza mkataba wake na mabingwa hao wa Ujerumani.

    Mkataba wa Kane unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao, lakini Bayern Munich ina nia ya kumbakisha mshambuliaji huyo kwa muda mrefu zaidi.

    Kane pia anafahamu kuwa uongozi wa klabu hiyo unataka asaini mkataba mpya, huku taarifa zikieleza kuwa makubaliano yanaweza kukamilika katika wiki zijazo.

    Mshambuliaji huyo alijiunga na Bayern Munich mwaka 2023 akitokea Tottenham Hotspur kwa ada ya pauni milioni 86.

    Tangu kuwasili kwake, Kane ameisaidia Bayern kutwaa mataji mawili ya Bundesliga na Kombe moja la Ujerumani.

    Pia alikuwa na mchango mkubwa kwa England katika Kombe la Dunia, akifunga mabao sita, huku akiwa ameifungia Bayern Munich jumla ya mabao 146 katika mechi 134 tangu ajiunge na klabu hiyo.

    Hata hivyo, ripoti zinaeleza kuwa Barcelona inaendelea kufuatilia hali yake, wakati baadhi ya klabu za Saudi Arabia zikisubiri fursa ya kumsajili pindi mkataba wake utakapomalizika.

    Soma Zaidi:

  6. Rufaa ya Senegal kupokonywa ubingwa wa AFCON kusikilizwa

    d

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo imepanga Oktoba 8 kuwa tarehe ya kusikiliza rufaa ya Senegal dhidi ya uamuzi wa kupokonywa ubingwa wa Mataifa ya Afrika wa mwaka 2025.

    Shirikisho la Soka Afrika lilibatilisha ushindi wa Senegal na kutangaza Morocco kuwa mabingwa wa mashindano hayo yaliyomalizika Januari, licha ya Senegal kushinda mchezo huo kwa bao 1 kwa 0.

    Mzozo ulizuka mwishoni mwa mchezo wakati Morocco ilipopewa penalti huku matokeo yakiwa bado 0 kwa 0.

    Wachezaji wa Senegal walitoka uwanjani kupinga uamuzi huo.

    Baada ya mchezo kusimama kwa dakika 17, wachezaji wa Senegal walirejea uwanjani, na Brahim Diaz akaifungia Morocco penalti waliyopewa.

    Mnamo Machi 25, Senegal iliwasilisha rufaa katika Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo ikitaka uamuzi wa CAF ubatilishwe na kombe la ubingwa lirejeshwe kwao.

    Katika uamuzi wake, CAF ilitangaza Morocco kuwa washindi kwa mabao 3 kwa 0 dhidi ya Senegal.

    Sasa Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo itasikiliza rufaa hiyo Oktoba 8 kabla ya kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu nani anayestahili kutambuliwa rasmi kama bingwa wa AFCON 2025.

    Soma Zaidi:

  7. Saudi Arabia yashambulia ngome za Wahouthi Hodeidah

    d

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia umetangaza kuwa operesheni yake dhidi ya Wahouthi imekamilika baada ya kushambulia kambi za kijeshi za kundi hilo kufuatia mashambulizi dhidi ya meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu.

    Msemaji wa muungano huo, Turki al Maliki, alisema kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa X kuwa Wahouthi walilenga meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu, jambo lililochochea muungano kujibu kwa kile alichokiita “jibu kali na la kuamua.” Kwa mujibu wa Al Maliki, mashambulizi hayo yalilenga maeneo yaliyokuwa

    Kwa mujibu wa chanzo cha kiusalama kilichozungumza na AFP, mashambulizi hayo yalilenga maeneo ya kijeshi na ngome zinazotumiwa na Wahouthi.

    Runinga ya Al Masirah inayomilikiwa na Wahouthi ilisema maeneo kadhaa katika mkoa wa Hodeidah yalishambuliwa, huku wakazi wa eneo hilo wakithibitisha kusikia milipuko mikubwa.

    Kundi la Wahouthi wa Yemen limetishia kulipiza kisasi dhidi ya Saudi Arabia siku ya Jumamosi, likiishutumu nchi hiyo kwa kulenga miundombinu ya kiraia. Hatua hiyo inaashiria kuongezeka kwa mivutano katika vita vinavyoendelea katika eneo hilo.

    Aidha, kundi hilo limetishia kulenga njia kuu za usafiri wa baharini za Saudi Arabia.

    Mashambulizi hayo yanajiri wakati mvutano wa usalama katika eneo hilo ukiendelea kuongezeka.

    Hivi karibuni Wahouthi walitangaza kuanzisha mzingiro wa baharini dhidi ya Saudi Arabia na kudai kulenga meli zinazohusishwa na taifa hilo.

    Soma Zaidi:

  8. Trump azitaka China na Urusi kutoingilia vita dhidi ya Iran

    d

    Chanzo cha picha, Reuters/File photo

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema marais wa China na Urusi wamemhakikishia kuwa hawataiuzia Iran silaha.

    Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema Rais wa China, Xi Jinping, alimweleza wakati wa mkutano wao wa hivi karibuni mjini Beijing kuwa China haitatoa wala kuuza silaha kwa Iran kwa hali yoyote.

    “Katika mkutano wetu wa hivi karibuni mjini Beijing, Rais Xi aliniambia kwamba hatatoa wala kuuza silaha kwa Iran kwa hali yoyote. Hilo linajumuisha pia kampuni za China,” aliandika Trump.

    Trump aliongeza kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin, pia alimpa ahadi kama hiyo.

    Akizungumzia msaada wa kijeshi kwa Ukraine, Trump alisema: “Watu wanafikiri siuzi silaha kwa Ukraine. Ninaziuza kwa nchi za NATO. Wanalipa bei kamili kwa silaha hizo na sijui wanazifanyia nini baadaye.”

    Trump pia alisema haamini kuwa China na Urusi zinahusika moja kwa moja katika vita dhidi ya Iran.

    “Mataifa hayo mawili makubwa ambayo mara nyingi hutajwa kuhusishwa na Iran, sidhani kama yanahusika. Kama yangekuwa yanahusika, hakika isingekuwa kwa maslahi yao wenyewe,” alisema.

    Hata hivyo, China na Urusi hazijatoa tamko rasmi kuthibitisha kauli za Trump kuhusu madai hayo.

    Soma Pia

  9. Trump asema Iran bado haiko tayari kufikia makubaliano na Marekani

    h

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema Marekani na Iran zinaendelea na mazungumzo ya kutafuta suluhisho la mgogoro kati ya mataifa hayo mawili, lakini akasisitiza kuwa Tehran bado haiko tayari kufikia makubaliano.

    Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu ya White House siku ya Ijumaa, Trump alisema: “Tunazungumza nao. Nafikiri wana nia ya dhati, na wako makini zaidi kuliko wakati mwingine wowote, lakini hilo halimaanishi tutafikia makubaliano. Tutaona kitakachotokea.”

    Kuhusu makubaliano ya ushirikiano wa nyuklia wa kiraia kati ya Marekani na Saudi Arabia, Trump alisema hatasonga mbele na utekelezaji wa makubaliano hayo hadi Saudi Arabia itakapokubali kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel kwa kujiunga na Makubaliano ya Abraham.

    Kauli hiyo inajiri siku chache baada ya Marekani na Saudi Arabia kutangaza makubaliano yatakayoiruhusu Riyadh kurutubisha urani na kujenga mitambo ya nyuklia kwa kutumia teknolojia ya Marekani, bila kufuata utaratibu wa ukaguzi wa haraka wa Umoja wa Mataifa ambao Washington imekuwa ikisisitiza utekelezwe kwa Iran.

    Hadi sasa, Saudi Arabia haijakubali kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia na Israel, jambo linalobaki kuwa moja ya vikwazo vikuu katika mazungumzo kati ya pande hizo.

    Unaweza kusoma;

  10. Hujambo na karibu kwa matangazo ya moja kwa moja ya tarehe 25/07/2026.