Trump asema ‘anapenda mfumuko wa bei’ wakati bei nchini Marekani zikiongezeka kwa kasi kubwa

Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa "anapenda mfumuko wa bei" baada ya bei nchini Marekani kupanda mwezi uliopita kwa kasi kubwa zaidi katika kipindi cha miaka mitatu.
Takwimu za Bureau of Labor (BLS) zilionesha kuwa bei ziliongezeka kwa asilimia 4.2 mwezi Mei ikilinganishwa na mwaka uliopita.
Hili ni ongezeko kutoka asilimia 3.8 mwezi Aprili. Kuongezeka huko kulichangiwa na kupanda kwa gharama za nishati kufuatia vita kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
"Ninapenda. Takwimu zilikuwa nzuri. Mnajua ninachopenda zaidi? Ninapenda mfumuko wa bei," Trump alisema akiwa Ikulu ya Marekani.
Hata hivyo, aliahidi kuwa bei hizo zinazopanda "zitashuka kwa kasi kubwa" mara tu vita na Iran vitakapomalizika. Baadaye siku hiyo, jeshi la Marekani lilifanya mashambulizi ya anga dhidi ya Iran.
Akizungumzia takwimu za mfumuko wa bei siku ya Jumatano, rais huyo alisema vikosi vya Marekani vilifanya operesheni za usiku na kuchukua "mamilioni ya mapipa" ya mafuta kutoka Iran, jambo ambalo alisema limechangia kushuka kidogo kwa bei za mafuta.
"Mgogoro huu ukimalizika... mtashuhudia bei ya mafuta ikishuka na kurudi katika kiwango ilichokuwa kabla ya vita," aliwaambia waandishi wa habari katika Ikulu ya Marekani.
Trump pia alirejelea safari yake katika jimbo la Iowa mapema mwaka 2026, akisema aliona petroli ikiuzwa kwa dola 1.85 kwa galoni moja, na kuongeza kuwa "tutarudi kwenye viwango hivyo hivi karibuni."
Hata hivyo, bei ya mafuta ghafi ya aina ya Brent crude bado inaendelea kuuzwa kwa kiwango cha juu zaidi ikilinganishwa na bei zilizokuwepo kabla ya vita kuanza.
Unaweza kusoma;













